WANAFUNZI WA SEKONDARI WASOMEA KATIKA VYUMBA VYA MAABALA


Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kasokola iliyopo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wanalazimika kusomea katika vyumba vya maabala vyenye kemikali za kisayansi zinazotumika kwa ajili ya masomo ya fikizikia,Kemia na baiolojia.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wameiomba serikali na wadau kujenga vyumba vya madarasa ili kuwaepusha na mazingira hatarishi walimu na wanafunzi.
Kwa upande wake Kaimu mkuu wa shule ya sekondari Kasokola Joel Mwandwanda amesema wanafunzi kusomea katika vyumba vya maabala kunatokana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo ambapo hata walimu wamegeuza maabala hizo na baadhi ya vyumba vya madarasa kuwa ofisi.
Kwa mjibu wa kaimu Mkuu wa shule hiyo yenye wanafunzi 415 iliyoanzishwa tangu mwaka 2008 ina upungufu wa walimu hasa katika masomo ya Sayansi ambapo kwa sasa kuna walimu wawili mmoja akifundisha hisababti na mwingine Kemia kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne.
Shule hiyo tangu mwaka 2008 ilipoanzishwa mpaka kufikia mwaka 2016 haikuwa na mwalimu wa sayansi hata mmoja suala ambalo lilikuwa gumu kwa wanafunzi hasa wanaofanya mitihani kwa vitendo katika masomo ya Fizikia,Kemia na Baiolojia kushindwa kufaulu vizuri.
Pia kaimu Mkuu wa shule hiyo amebainisha changamoto nyingine ambazo ni kikwazo kwa shule hiyo kuwa ni uahaba wa walimu wa sayansi,uhaba wa vyumba vya madarasa na kusababisha wanafunzi zaidi ya wastani unaotakiwa kuwa katika chumba kimoja.
Hata hivyo licha ya changamoto hizo,shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika mtiohani wa kidato cha nne.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA