Posts

Showing posts from March 10, 2018

MWANAMKE AFARIKI DUNIA BAADA YA KUTELEKEZWA NA MUMEWE,WANAWAKE WALAANI

Image
Wanawake wa Mtaa wa Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wamelaani vikali kitendo cha Abdalla Ibrahim Mkazi wa mtaa huo kumtelekeza mkewe Rosemary Robert Ismail mpaka kusababisha kifo chake kwa kutompatia huduma baada ya kuugua kwa muad mrefu. Wanawake hao wamesema kitendo ambacho amekifanya Bw.Ibrahimu ambaye ni mlinzi wa kampuni moja mjini Mpanda ni ukatiri wa hali ya juu.

WADAU WA ELIMU WACHANGIA ZAIDI SHILINGI MIL.152 KWA AJILI YA SEKTA YA ELIMU

Image
Zaidi ya Shilingi milioni 152 zimechangwa na wadau wa elimu wilayani Tanganyika mkoani Katavi,ili kutatua matatizo ya miundombinu ya elimu wilayani humo. Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhaga ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ambayo imefanyika Mpanda Mjini,ametoa wito kwa wadau wengine kuendelea kushirikiana na serikali ili kuleta maendeleo.