Posts

Showing posts from April 18, 2018

MGANGA MKUU JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA

MHAKAMA ya  Wilaya ya  Mpanda  Mkoani  Katavi   imemuhukumu mganga mkuu wa  Zahanati ya  Kasekese  Wilaya ya  Tanganyika  Martin  Mwashamba  (27)kifungo cha  miaka  30 jela baada ya kumtia hatiani kwa kosa la mbaka na kumpa  mimba  wanafunzi wa  dasasa la  sita  wa  shule ya  Msingi  Kasekese mwenye  umri wa miaka 15  jina  lake limehifadhiwa. Hukumu  hiyo ilitolewa  jana   na   Hakimu  mkazi wa  Mahakama ya  Wilaya hiyo  Odira  Amwol   baada ya  Mahakama  kuridhika  na  ushahidi  uliotolewa  Mahakamani  hapo  na   upande wa  mashitaka. Awali katika  kesi  hiyo  mwendesha  mashtaka   Mwanasheria wa   Serikali Mkoani Katavi  Gregoli  Mhagwa  alidai   Mahakamani  hapo  kuwa   mshitakiwa  alitenda  kosa  hilo  Julai  2  mwaka  jana   Kijijini  hapo. Alieleza  Mahakamani  hapo siku  hiyo ya  tukio  mshitakiwa  alimbaka   mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa    darasa la  sita wa shule   ya   Msingi  Kasekese mwenye  umri wa  miaka   15 huku  akijua  kufanya  hivyo ni  kosa. Upande

TRA KATAVI KUHAKIKI TIN NAMBA

Image
Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoani katavi,imeanza kuhakiki namba za utambuzi(TIN NAMBA) kwa wafanya biashara waliosajiliwa katika biashara zao. Meneja wa TRA mkoani Katavi Enos Mgimba amesema zoezi la uhakiki hili ambalo limeanzia leo Aprili 18,2018 katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda baadaye litaendshwa katika maeneo mengine ya Mkoa. Mgimba ametaja baadhi ya faida ya utambuzi wa TIN   NAMBA kwa TRA kuwa ni pamoja na mamlaka kuwa na taarifa sahihi za wafanyabiashara ili hali kukusanya mapato na kusaidia katika utatuzi wa changamoto mbalimbali za kibiashara. Baadhi ya wafanyabiashara ambao wamefika katika zoezi hilo wamesema zoezi hilo lina faida kwao ikiwemo kutambulika katika biashara anayoifanya. Halmashauri 5 za Mkoa wa Katavi zinazotakiwa kufanyiwa uhakiki ni Manispaa ya Mpanda na Nsimbo zinazopatikana Wilayani Mpanda,Mlele na Mpimbwe zinazopatikana Wilayani Mlele na ,Mpanda inayopatikana Wilayani Tanganyika. Kwa mjibu wa Meneja Enos Mgimba,Jumla ya wafanyabia