Posts

Showing posts from November, 2015

DAWA ZA MAGONJWA YASIYOKUWA YANAPEWA KIPAUMBELE KUANZA KUGAWIWA KESHO KATAVI

Na.Issack Gerald-MPANDA. JAMII Mkoani Katavi imetakiwa kuzingatia utaratibu wa wataalamu wa afya juu ya matumizi ya dawa za magonjwa yasiyokuwa yanapewa kipaumbele Mkoani   hapa.

WAKAZI MKOANI KATAVI WANAOZUNGUKA HIFADHI WATAKIWA KUTOFANYA SHUGHULI YOYOTE HIFADHINI

Na.Issack Gerald-MPANDA Wananchi wanaoishi karibu na hifadhi mbalimbali Mkoani Katavi wameshauriwa   kutofanya shughuli yoyote ndani ya hifadhi pamoja na   kuzingatia sheria   ya uhifadhi ili kuendelela kuzilinda hifadhi hizo.

WAZAZI,WALEZI KATAVI WAASWA KUWAPELEKA VIJANA WAO KATIKA VYUO KUPATA SOKO LA AJIRA

Na.Issack Gerald-MPANDA WAZAZI na walezi mkoani katavi wameshauriwa kuwapeleka vijana wao katika vyuo mbalimbali vya mafunzo ya ufundi stadi VETA   ili waweze kupata elimu itakayowasaidia kuingia katika soko la ajira ikiwa pamoja na kujiajiri wenyewe pindi wamalizapo masomo yao.

WAKAZI MPANDA WAASWA KUJENGA NYUMBA BORA KUJIKINGA NA MVUA ZA ELNINO

Na.Issack Gerald-MPANDA WAKAZI wa wilaya ya Mpanda mkoani Katavi, wameshauriwa kujenga nyumba bora ili kuepukana na madhara yanayoweza kusababishwa na mvua zinazosadikika kuwa za elnino.

VYAKULA VYA KUTEMBEZA MITAANI VYAPIGWA MARUFUKU MPANDA

Na.Issack Gerald-MPANDA HALMASHAURI ya Manispaa ya Mpanda imepiga marufuku   uuzaji wa   vyakula vya kutembeza, kama vile uji, barafu, juice na vyakula vinavyouzwa katika maeneo yasiyo rasmi.

RAIA WAPYA KAMBI YA KATUMBA WAENDELEA KUFURAHIA KUWA WATANZANIA

Na.Issack Gerald-MPANDA MKUU wa makazi ya Katumba yaliyopo wilayani Nsimbo mkoani Katavi   Bw. Athuman Igwe, amesema jumla ya wakimbizi waishio katika wilaya hiyo ni elfu kumi na tisa elfu mia saba sabini na tatu, na waliopata uraia ni sitini na mbili elfu huku walio na vyeti ni hamsini na saba elfu.

WATENDAJI WALIOGOMA KUHUDHURIA KIKAO CHA MKURUGENZI WILAYA YA MPANDA KUKABILIWA NA ADHABU

Na.Issack Gerald-MPANDA HALMASHAURI ya wilaya ya Mpanda imeagiza kuchukuliwa hatua kwa watendaji wa kata na vijiji walioshindwa kuhudhuria kikao cha kazi kilichoitishwa na mkurugenzi bila taarifa.

KAKESE,MWAMKURU WATAHADHARISHWA KIPINDUPINDU WAASWA KUDUMISHA USAFI

Na.Issack Gerald-MPANDA. WANANCHI wa Kata ya Kakese na Mwamkulu katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wametakiwa kuzingatia usafi ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu.

UONGOZI SOKO KUU MPANDA WAKANUSHA KUTOZA USHURU MARA MBILI,KUTO TOA RISITI NA UNYANYASAJI

Na.Issack Gerald-MPANDA Uongozi wa soko kuu lililopo Wilayani Mpanda Mkoani Katavi umekanusha madai yaliyotolewa na wafanyabiashara wa soko hilo kuhusu kutozwa ushuru mara mbili na wasimamizi wa soko hilo.

UZINDUZI MATUMIZI YA MIZANI,TAASISI ZA SERIKALI NA BINAFSI ZAASWA KUHAMASISHA MATUMIZI YA VIPIMO HALALI KATIKA BIASHARA

Image
Mmoja wa wakazi wa Mpanda akionesha kauli mbiu ya hapa kazi tu siku ya uzinduzi wa wakala wa vipimo katika viwanja vya soko la Buzogwe Manispaa ya Mpanda (PICHA na Issack Gerald) Mkuu wa Wilaya ya Mlele Kanal Issa Seleman Njiku akimkabidhi mzani mfanyabiashara mdogo kama ishara ya kuzindua matumizi ya mizani Mkoani katavi yaliyofanyika leo katika viwanja vya soko la Buzogwe (Picha Issack Gerald) Kikao cha wakala wa vipimo na waandishi wa habari,katikakati ni Irene John Kaimu meneja wa Sehemu ya elimu habari na mawasiliano wa wakala wa vipimo kutoka makao makuu Dar Es salaam,Mwenye T-shirt Nyekundu ni Moses Ezekiel Ntungi,Mratibu wa Programu ya Ukopeshaji mizaniaMkoani Katavi  na aliyevaa koti ni Abnery Amos Nzaga Meneja wa Mkoa wakala wa vipimo Rukwa na Katavi (PICHA NA Issack Gerald) Baadhi ya wafanyabiashara katika uzinduzi wa matumizi ya vipimo(mizani) katika biashara (PICHA na Issack Gerald) Na.Issack Gerald-MPANDA Taasisi binafsi na serikali ziw

MKURUGENZI APEWA AGIZO KUSIKILIZA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA SOKO LA BUZOGWE

Na.Issack Gerald-MPANDA Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda amepewa siku moja kuhakikisha anafika soko la Buzogwe kuchunguza changamoto za ukosefu wa umeme,ulinzi wa biashara na maji zinazowakabili wafanyabiashara waliopo katika soko hilo.

WANNE MBARONI KATAVI AKIWEMO MWENYE NYARA ZA SERIKALI ZENYE THAMANI YA SHILINGI MIL.60

Na.Issack Gerald-MLELE Jeshi la Polisi Wilayani Mlele Mkoani Katavi kwa kushirikiana na askari wa Hifadhi ya Taifa ya wanyama Pori (TANAPA) ,linawashikilia watu wanne akiwemo mmoja ambaye amekamatwa na jino moja na mikia miwili ya Tembo vikiwa na thamani ya Shilingi milioni 60.

WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI KATAVI WATAKIWA KUEPUKA MAZINGIRA YA UKATIRI

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA . WANAFUNZI wa Shule za Msingi na Sekondari Mkoani Katavi wametakiwa   kuepuka mazingira yanayopelekea   vitendo ya ukatili na unyanyasaji na   kuzingatia masomo.

WAKALA WA VIPIMO TANZANIA KUZINDUA MATUMIZI YA VIPIMO KESHO MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald-MPANDA Wakala wa vipimo Tanzania Kesho wanatarajia kuzindua na kukopesha mizani kwa wafanyabiashara wadogo Mkoani Katavi kwa ajili ya kuondokana na hasara zinazotokana na kuuza bidhaa mbalimbali pasipo kutumia vipimo halali.

UONGOZI HOSPITALI YA WILAYA MPANDA WALALAMIKIWA KWA KUTOA HUDUMA DUNI KWA WAGONJWA

Na.Issack Gerald-MPANDA BAADHI ya wakazi wa Manispaa ya Mpanda wameulalamikia uongozi wa hospital ya wilaya ya Mpanda kwa kutoa huduma isiyoridhisha.

WAKAZI KATAVI WATAKIWA KUWA TAYARI KWA USAFI DESEMBA 9

Na.Issack Gerald-MPANDA. WAKAZI Katika Mkoa wa Katavi wametakiwa Kuwatayari Kushiriki Katika zoezi la Kufanya usafi wa Mazingira litakalofanyika Nchi nzima December 9 Mwaka huu.

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI PINGAMIZI LA POLISI

Na.Mwandishi wetu-Mwanza. Mahakama kuu kanda ya mwanza imetupilia pingamizi la  polisi kuzuia  waombolezaji kufanya ibada ya kuuaga mwili wa aliyekuwa mwenyekiti wa chadema mkoa wa geita Afonce Mawazo aliyeuwawa nov.14 mwakahuu kwa kukatwa mapanga.

WAKAZI MANISPAA YA MPANDA WALIA NA UKOSEFU WA MAJI SAFI NA SALAMA

Na.Issack Gerald-MPANDA Wakazi wa kata ya Makanyagio katika Manispaa ya   Mpanda Mkoani katavi wameiomba mamlaka ya maji safi na salama Manispaa ya Mpanda kutafuta ufumbuzi wa kuondoa kero ya kukosekana kwa maji safi na salama kwa wananchi hao.

WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAANZA MTIHANI WA MOCK KIKANDA

Na.Issack Gerald-MPANDA WANAFUNZI wa kidato cha sita katika Manispaa ya Mpanda wameanza kufanya mtihani wa mock.

VIONGOZI NGAZI YA CHINI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA MASLAHI YA UMMA

Na.Issack Gerald-NSIMBO VIONGOZI wa ngazi ya chini wametakiwa kufanya kazi kwa maslahi ya umma ili kuendana na Kasi ya Rais Dr Jonh Pombe Magufuli.

WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUKAMATWA NA NYARA ZA SERIKALI

Na.Issack Gerald-MPANDA WATU Wawili wanaokabiliwa na mashtaka ya kukamatwa na nyara za serikali, wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Mpanda na   kusomewa mashtaka.  

MGOGORO WA WAFANYABIASAHARA WA MATUNDA SOKO LA MPANDA HOTEL WAMALIZIKA

Na.Issack Gerald-MPANDA Wafanyabiasahara wa matunda katika soko la Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda,wamewapongeza viongozi wa Manispaa,madiwani , maafisa masoko na Bibi afya   kwa kuwaruhusu kuuza matunda yao katika eneo wanalolitaka baada ya kufanya usafi wa kuridhisha.

WAZIRI MKUU KASSIMU MAJALIWA NI NANI?SOMA HAPA

Image
  Waziri Mkuu wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa Waziri Mkuu mteule wa Tanzania, Kassim Majaliwa, alizaliwa Disemba 22, 1960 Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

MAJALIWA KASSIMU MAJALIWA WAZIRI MKUU WA 11 TANZANIA TANGU UHURU WA TANGANYIKA

Image
  Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwa katika kikao cha kwanza katika mkutano wa kwanza wa bunge la 11 kumchagua Waziri mkuu wa Tanzania na Naibu Spika Na.Mwandishi wetu-DODOMA Mbunge wa Ruangwa Majaliwa Kassim Majaliwa ameidhinishwa na Bunge la Tanzania kuwa waziri mkuu mpya wa Tanzania.

MANISPAA YA MPANDA KUFANYA TAFRIJA KESHO KUWAPONGEZA WALIMU KWA KUFAULISHA WANAFUNZI DARASA LA SABA NA KUWA NAMBA MOJA KITAIFA

Na.Issack Gerald-Mpanda Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani katavi inatarajia kufanya tafrija ya kuwapongeza walimu kwa matokeo mazuri ya darasa la saba yaliyopelekea Manispaa ya Mpanda kushika nafasi ya kwanza kitaifa 2015.

KUUWAWA BODABODA KATAVI,KWAWAAMSHA POLISI KATAVI,WAAMUA KUITISHA MKUTANO WA BODABODA

Na.Issack Gerald-MPANDA Kufuatia kukithiri kwa vitendo vya mauaji ya waendesha pikipiki Mkoani Katavi,Mkuu wa usalama barabarani ameitisha kikao kinachotarajia kufanyika kesho kujadili kwa kina suala hilo.

WAFANYABIASHARA WA MATUNDA SOKO LA MPANDA HOTELI WANAOUZIA CHINI WAGOMA KUOANDOKA

Na.Issack Gerald-Mpanda Wafanyabiashara wa bidhaa katika soko la Mpanda hoteil lililopo halmashauri ya mji Mpanda wamegomea agizo lililotolewa na Mwenyekiti wa soko hilo bwana Boniphace Mganyasi la kutaka kuhamisha bidhaa zao chini na kupeleka katika vichanja vya ndani.

WAZAZI,WALEZI WATAKIWA KUTOWAFICH AWATOTO WENYE ULEMAVU

Image
  Baadhi ya watoto walemavu wakisikiliza maelezo ya walimu wao,walimu hawapo pichani Na.Issack Gerald-MPANDA Wazazi na walezi wilayani Mpanda Mkoani Katavi wametakiwa kuacha tabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu mbalimbali badala yake wawapeleke shule kupata elimu jumuishi itakayo wasaidia katika maisha yao.

WAKAZI KATAVI WAHIMIZWA USAFI

Na.Issack Gerald-MPANDA. Wananchi Mkoani Katavi wametakiwa kuzingatia usafi wa Mwili Mazingira na Vyakula ili kujikinga na Maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu.

SPIKA BUNGE LA TANZANIA KUCHAGULIWA KESHO,SITTA NJE KINYANG'ANYIRO

Image
  Jengo la Bunge Mjini Dodoma Na.Mwandishi wetu-DODOMA Wabunge wateule wa bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanatarajia kumchagua Spika wa Bunge hilo kesho Mjini Dodoma.

KATA YA SITALIKE KUKUSANYA MAPATO KUTOKA MIGODINI NA HIFADHINI

Na.Issack Gerald-NSIMBO UONGOZI wa Kata ya Sitalike wilayani Nsimbo mkoani Katavi, unatarajia kukusanya mapato kutoka kwa wawekezaji wa migodi pamoja na hifadhi ya taifa ili kuchangia maendeleo ya kata hiyo.

HALMASSHAURI YA MJI NJOMBE YAWAONYA WALIMU WAKUU WATAKAOFELISHA WANAFUNZI

Na.Mwandishi wetu-NJOMBE Halmashauri ya mji wa njombe imesema itaendelea kutoa adhabu za kuwa vua vyeo walimu wakuu ambao shule zao zinafelisha wananfunzi kuufikia wastani waliojiwekea ili kukuhakikisha halmashauri hiyo inangara kielimu kwa kufikia ufaulu wa juu.

UKEKETAJI WA WANAWAKE WAPUNGUA LOLIONDO ARUSHA

Image
  Pichani ni mjumuiko wa wakunga wa Jadi, Waganga wa tiba asili, viongozi wa dini, waandishi wa habari na wahamasishaji afya jamii wanaohudhuria warsha hiyo inayoendelea wilayani Ngorongoro. Washiriki wa warsha hiyo wakiwa kwenye kazi za vikundi. Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia ni Afisa Maendeleo ya Jamii, Teresia Irafay akifungua warsha ya wiki moja ya mafunzo juu ya elimu ya Afya ya Uzazi na Maadili iliyojumuisha wakunga wa Jadi, Waganga wa tiba asili, viongozi wa dini, waandishi wa habari na wahamasishaji afya jamii iliyowaleta pamoja wadau mbalimbali katika ngazi ya vitongoji, vijiji na wilaya kujifunza namna ya kufanya kazi shirikishi ili kuleta mabadiliko katika jamii inayofanyika katika hoteli ya Domel-Wasso, tarafa ya Lolilondo katika wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha. Na.Mwandisi waetu-ARUSHA IDADI ya wanawake wanaokeketwa Loliondo wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha,imepungua kufikia asilimia 7

WABUNGE WATEULE WA BUNGE LA TANZANIA KUANZA KUSAJILIWA LEO

Image
  Baadhi ya wabunge la Tanzania wakiangalia mandhali ukumbi  bungeni Mjini Dodoma Na.Mwandishi wetu-DODOMA Wabunge wateule wa bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanatarajia kujisajili leo tayari kwa vikao muhimu vya kwanza vya Bunge wiki ijayo.

WATANZANIA WAISHIO NCHINI THAILANDA WACHAGUA VIONGOZI WAO

Image
  Watanzania waishio mjini Bangkok nchini Thailand wakipata chakula baada ya kufanya uchaguzi Na.Mwandishi.BANGKOK Jumuiya ya watanzania waishio nchini Thailand (TIT) imekutana na kujadiliana mambo mbalimbali ya jinsi gani wanaweza kusaidiana katika mambo mbalimbali.

VIJANA MPANDA WAELEZA WALIVYONUFAIKA NA MAADHIMISHO YA SIKU YA VIJANA DUNIANI

Image
  Vijana katika kongamano Mjini Dodoma katika maadhimisho siku ya vijana Duniani Na.Issack Gerald-MPANDA Vijana katika Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda walioshiriki kongamano la wiki ya Vijana Oktoba 14 mwaka huu,wamesema kuwa walinufaika sana na mafunzo mbalimbali ambayo wanatarajia kuyatumia na kufanikiwa katika shughuli za kijasiliamali.

ASKARI WA WANYAMAPORI KATAVI WALALAMIKIWA KWA UDHALILISHAJI WA RAIA NSIMBO

Na.Masoud Mmanywa-Nsimbo WAKAZI wa kijiji cha Mtisi Kata ya Stalike wilayani Nsimbo mkoani Katavi, wamewalalamikia askari wa Wanyamapori kwa kuwapiga na kuwajeruhi kwa madai ya kuwakuta wakilima katika eneo la hifadhi ya msitu.

MIL.80 ZATUMIKA KUSAIDIA KAYA 62 ZILIZOATHIRIWA NA MVUA,WAFANYABIASHARA NAO KUFANYIWA TATHMINI

Na.Issack Gerald-SUMBAWANGA Zaidi ya Shilingi Milioni 80 zimetumika kuwasaidia wahanga wa mvua iliyombatana na upepo Mkali Oktoba mosi mwaka huu.

WAFANYABIASHARA,WANUNUZI WAILALAMIKIA SERIKALI KUPANDISHA BEI YA BIDHAA

Na.Issack Gerald-MPANDA BAADHI ya Wanunuzi na wafanyabiashara wadogo wadogo wilayani Mpanda mkoani Katavi wameilalamikia serikali kutokana na kupandisha bei za bidhaa nchini kiasi kinachowafanya washindwe kuyamudu maisha yao.

WAKULIMA WAOMBA PEMBEJEO ZA KILIMO ZILETWE MAPEMA

Na. Lutakilwa Lutobeka - MPANDA Kucheleweshwa kwa pembejeo kwa wakulima imeelezwa kuwa ni sababu inayozorotesha sekta ya kilimo wilayani Mpanda, mkoani Katavi.

RUKWA WAJIPANGA KUHIFADHI MAZINGIRA

NA.Issack Gerald-SUMBAWANGA Mkoa wa Rukwa Umepanga kupanda miti milioni Tano na laki tano katika Halmshauri zake kwa mwaka wa 2015/2016 lengo likiwa ni kuhifadhi mazingira.