Posts

Showing posts from June 6, 2018

MSITU WA TONGWE MAGHARIBI WENYE SOKWE ZAIDI YA 800 SASA MIKONONI MWA HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Muhando akizungumza na wananchi wa kijiji cha Katuma(PICHA NA Issack Gerald) Sokwe moja ya wanyama wanaopatikana msitu wa Tongwe Magharibi Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Kapanga wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Mpanda Salehe Muhando(Hayupo pichani)(PICHA NA Issack Gerald) Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Salehe Muhando,amesema wizara ya maliasili na utalii imekubali msitu wa Tongwe Magharibi kumilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda kutoka katika mamlaka ya wizara hiyo. Muhando amebainisha hatua hiyo kupitia mikutano ya hadhara katika vijiji vya Kapanga na Katuma Kata ya Katuma lengo likiwa ni kuelimisha kutunza msitu huo wenye zaidi ya sokwe 800 kwa ajili ya faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.