Posts

Showing posts from December, 2015

WAZIRI MKUU AHITIMISHA ZIARA YA SIKU MBILI KIGOMA ATAJA MKAKATI WA SERIKLAI KUPANUA BANDARI ZIWANI TANGANYIKA

Image
Na.Issack Gerald-KIGOMA WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Halimashauri ya Manispa Kigoma Ujiji kwa kubuni miradi mbalimbali ya biashara katika ziwa Tanganyika na   tekinolojia mpya ya kukausha dagaa wanaovuliwa katika ziwa hilo.                                                Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akikagua dagaa wanaokaushwa kitalaam kwa kutumia jua  wakati  alipozindua soko na mwaro wa kisasa wa samaki wa Kibirizi  mjini Kigom. Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

WAKAZI LAKI MBILI (200,000) WATESWA NA NJAA JIMBO LA UYUI TABAORA BAADHI HAWANA HATA UWEZO WA KUNUNUA KWA BEI NAFUU

Image
Na.Issack Gerald-Tabora Watu  zaidi ya 200,000 katika jimbo la Igalula Wilayani Uyui Mkoani Tabora wanakabiliwa na uhaba wa chakula ambapo zaidi ya wakazi 20,000 wakiwa hawana uwezo wakununua hata chakula cha kwa bei nafuu.

KATIBU TAWALA KIGOMA APEWA SIKU MBILI KUKABIDHI TAARIFA YA MAANDI YA UBADHIRIFU KWA WAZIRI MKUU MAJALIWA

Image
Na.Ofisi ya mawasiliano ya Waziri Mkuu WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku mbili kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Eng. John Ndunguru kukamilisha uchunguzi wake na kumpatia taarifa ya maandishi juu ya tuhuma ubadhirifu wa fedha za umma unaohusisha uuzwaji wa jengo la KIGODECO na viwanja 12 vya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambao unadaiwa kukiuka taratibu.                                                                               Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizindua soko na Mwaro wa samaki wa Kibirizi mjini Kigoma .Kushoto ni Mkuu wa Mkoa huo Issa Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizindua soko na Mwaro wa samaki wa Kibirizi mjini Kigoma Desemba 28 , 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MTAFARUKU BAINA YA MANESI NA WANANCHI WANAOHITAJI HUDUMA HOSPITALINI MLELE.

Na.Suzan Kanenka-Mlele Upungufu wa Manesi(wauguzi) katika kitengo cha huduma ya afya ya uzazi katika hospitali ya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi,umezua mtafaruku baina ya wahudumu wa kitengo hicho na wananchi wanaostahili huduma hiyo.

WANANCHI KATAVI WAIOMBA SERIKALI YA AWAMU YA TANO CHINI YA MAGUFULI KUUNDA MAHAKAMA YA KIFAMILIA

Na.Agness Mnubi-MPANDA. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya tano Ya Dk. John Pombe Maghufuli   imeombwa kuunda Mahakama ya Kifamilia itakayojihusisha na   kushughulikia vitendo vya ukatili na unyayasaji wa kijinsia.

BREAKING NEWS : MTOTO (16) ALALA NJE TANGU UTOTONI CHANZO WAZAZI KUMFUKUZA NYUMBANI,TAASISI ZA KUPINGA UNYANYASAJI ZAINGILIA KATI.

Na.Agness Mnubi-MPANDA. MTOTO anayefahamika kwa jina la Adamu Ramadhan mkazi wa Manispaa ya Mpanda, yuko katika hatari ya kuathirika kisaikolojia kutokana na vitendo vya kikatili.

UKAMATWAJI NYARA ZA SERIKALI KATAVI WAKITHIRI,WENGINE WAWILI WADAKWA NA KUSHIKILIWA NA POLISI,BAADHI YA WAKAZI KATAVI WATOA YA MOYONI.

Na.Issack Gerald-Mpanda,Katavi Jeshi la polisi Mkoani Katavi,linawashikilia watu watatu baada ya kukamatwa wakiwa na vipande 12 vya meno ya tembo vikiwa na uzito wa kilogramu 11 ambapo thamani yake ni   shilingi Milioni miamoja na ishirini(120,000,000).

WANANCHI KATAVI WAPONGEZWA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari,ametoa pongezi kwa wananchi Mkoani Katavi,kwa kuendelea kudumisha amani katika msimu wa sikukuu za   Maulid na Krismasi.                                              Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi-Dhahiri Kidavashari

ANASWA NA NYARA ZA SERIKALI 38 KATAVI BAADHI NI PUA YA NGURUWE PORI NA KINYESI CHA FISI KWA UNDANI ZAIDI HAPA HAPAP5 TANZANIA

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Vitusi Chomba(36) mkazi wa Kijiji cha Senkwa Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi amekamatwa akiwa na nyara mbalimbali za serikali ikiwemo pua ya nguruwe pori.                                       Kamanda wa polisi Katavi-Dhahiri Kidavashari

BAADHI YA WAMILIKI WA VITUO TIBA ASILIA NA TIBA MBADALA MPANDA WAZUNGUMZIA ZUIO LA SERIKALI KUWEKA MATANGAZO REDIONI

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA Baadhi ya wamiliki wa vituo vya tiba asilia na Tiba Mbadala Wilayani Mpanda Mkoani Katavi wamesema kuwa Serikali Ya Tanzania haijakosea kusitisha utangazaji wa vituo hivyo katika vyombo vya habari kwa kuwa serikali imesimamia sheria za nchi.                                                       ALOVERA Miongoni mwa mimea inayotibu baadhi ya magonjwa

SERIKALI YA WILAYA YA MLELE KWENDA KWA WAZIRI KUPATA UHAKIKA LINI HOSPITALI ITAJENGWA

Na.Issack Gerald-MLELE SERIKALI ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi, imesema inatarajia kwenda kumuona Waziri wa Afya ili kupata uhakika lini wananchi waliotoa ardhi yao kujengwa hospitali ya wilaya hiyo watalipwa fidia zao.

MATUKIO YA WIKI MKOANI KATAVI NA TANZANIA KWA UJUMLA DESEMBA 21-26,2015 NA P5 TANZANIA YA ISSACK GERALD BATHROMEO

 NA.ISSACK GERALD BATHROMEO MAUAJI KATAVI Posted By: Issack Gerald | At: Monday, December 21, 2015 Na.Issack Gerald- Katavi Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la   KAZIMIRI MASUMBUKO(49) MKAZI NA MKULIMA WA MISANGA aliuawa kwa kuchomwa kitu chenye ncha kali sehemu za mgongoni, mkononi, mkono wa kushoto na kidevuni na watu wasiofahamika Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo,Kmanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari,amesema tukio hilo limetokea jana Jumapili tarehe 20.12.2015 majira ya saa katika kitongoji cha Misanga Kata na Tarafa ya Mwese Wilayani Mpanda Mkoani Katavi. Kamanda Kidavashari amesema kuwa, siku ya tukio hilo,watuhumiwa wasiofahamika kwa sura wala idadi yao walifika nyumbani kwa marehemu wakakuvunja mlango na kuingia moja kwa moja hadi chumbani kwa marehemu na kumpeleka sebureni kwake kisha kutekeleza mauaji hayo na kutokomea kusikojulikana . Mpaka sasa chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika. Hata hivyo Upelelezi wa shauri hili unaend

WATATU KATAVI WASHIKILIWA NA POLISI KWA KUKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI

Na.Issack Gerald-Mpanda Jeshi la polisi Mkoani Katavi linawashikilia watu watatu kutokana na kukamatwa na nyara za serikali ambazo wamezipata kinyume na sheria.

KAMANDA WA POLISI MWANZA ATOA TAARIFA YA ASKARI KUMUUA KWA RISASI ASKARI MWENZAKE

NA.Mwandisi wetu-MWANZA Askari mmoja  wa jeshi la Polisi mkoani Mwanza  jana amefyatua risasi na kumuua asikari mwenzake kisha nayeye kujipiga risasi na kufariki dunia katika lindo la benki ya posita jijini mwanza huku chanzo cha tukio hilo kikiwa hakija julikana.

AKIMBIA MKONO WA POLISI KUKWEPA KUKAMATWA KWA KOSA LA KUMILIKI SILAHA KINYUME NA SHERIA

Na.Issack Gerald-Mpanda Jeshi la polisi Mkoani Katavi linamtafuta mtu mmoja aliyekimbia akikwepa kukamatwa na polisi kutokana na kumiliki silaha aina ya gobore  kinyume na sheria.

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI AKICHIMBA DHAHABU NSIMBO KATAVI

Na.Issack Gerald-Mpanda Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina Mateo Robert(33) mchimbaji mdogo mkazi wa Mbeya-Songwe,amefariki dunia baada ya kuangukiwa na lundo la udongo akiwa kwenye shimo (LONG BASE) wakati akichimba madini ya dhahabu.

BODABODA MPANDA WAZUNGUMZIA MIUNDOMBINU MIBOVU YA BARABARA INAVYOATHIRI UCHUMI WAO

Na.Issack Gerald-MPANDA Miundombinu mibovu ya barabara hususani kipindi hiki cha masika imeathiri uchumi wa waendesha pikipiki katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Matavi.

WAKUU WA MIKOA,WILAYA NA WAKURUGENZI HALMASHAURI NCHINI WATAKIWA KUDHIBITI MIGOGORO YA ARDHI

Image
Na. OFISI YA WAZIRI MKUU,   WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa wanaongeza udhibiti na usimamizi wa migogoro ya  ardhi kwenye maeneo yao husika.                                                                  Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majliwa akisalimia na waakazi Jimboni Kwake Ruangwa

BREAKING NEWS : KAIMU MKURUGENZI WA TAASISI YA SARATANI YA OCEAN ROAD ASIMAMISHWA KAZI

Image
Na.Ofisi ya Waziri-DAR ES SALAAM. Kaimu mkurugenzi wa taasisi ya saratani ya Ocean Road Dk.Diwani Msemo amesimamishwa kazi.                                                        Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu

MKURUGENZI MKUU RAHCO ASIMAMISHWA KAZI

Image
Na.OFISI YA MAWASILIANO YA IKULU. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk.John Magufuli amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli Tanzania (RAHCO), Benhadard Tito.                                                 Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli

MKURUGENZI HALMSHAURI YA WILAYA YA KALAMBO,ASIKITISHWA NA HALI YA ELIMU MKOANI RUKWA

Na.Issack Gerald-SUMBAWANGA MKURUGENZI   Mtendaji wa   Halmashauri ya wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa Bw. Bensoni Kilagi,amesema hajaridhishwa na matokeo ya darasa la nne na darasa la saba kwa mwaka 2015 mkoani humo.

MEYA MANISPAA YA MPANDA AOMBA HOSPITALI YA WILAYA YA MPANDA KUHARAKISHWA KUWA MALI YA MANISPAA

Image
Na.Meshack Ngumba-MPANDA SERIKALI imeombwa Kuharakisha Mchakato wa Kuibadilisha hospitali ya Wilaya Kuwa hospitali ya halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ili Kusogeza huduma za afya kwa wakazi wa Manispaa hiyo.                                                           Baadhi ya majengo Hospitali ya Wilaya Mpanda

WAZIRI MKUU ASEMA HANA KINYONGO NA MTU YEYOTE,ASEMA ITIKADI ZA SIASA ZILIISHIA OKTOBA 25

Image
Na.OFISI YA WAZIRI MKUU. WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema hana kinyongo na mtu yeyote kwa sababu alitangaza msamaha siku aliyokabidhiwa cheti kuwa mbunge wa jimbo la Ruangwa na kusisitiza kuwa siasa ziliisha tangu Oktoba 25, mwaka huu.                                        Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akizungumza na Wakazi Mkoani Lindi

BUNGE NCHINI BURUNDI NA BALAZA LA SENATE NCHINI HUMO WAKUTANA KUJADILI HALI YA USALAMA BURUNDI

Na. Prosper Kwigize Bujumbura, Burundi Bunge la Jamhuri ya Burundi kwa pamoja na Baraza la SENATE leo wamekutana pamoja jijini Bujumbura kujadili hali ya usalama.

BIL.137 KUGHARIMIA ELIMU BURE JANUARI HADI JUNI 2016

Image
NA:OFISI YA WAZIRI MKUU -DAR ES SALAAM SERIKALI imekwishatenga kiasi cha sh. bilioni 137 kwa ajili ya kugharamia utoaji wa elimu ya bure kuanzia Januari hadi Juni, mwakani.                                                                              Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa

WAZAZI NA WALEZI WATAKIWA KUTAMBUA HAKI ZA MTOTO KUZUIA UKATIRI

Na.Agness Mnubi-MPANDA. WAZAZI na Walezi mkoani Katavi wametakiwa kutambua umhimu wa haki za watoto na kuepuka Mazingira yanayopelekea ukatili na unyanyasaji kwa watoto hao.

WAWILI MBARONI AKIWEMO KARANI WA CHUO CHA MAENDELEO MSAGINYA ,KWA SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI KATAVI

Image
Na.Issack Gerald- Katavi Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linawashikilia watu wawili akiwemo   ASHURA MSAGUSI(30) Karani wa chuo cha Maendeleo Msaginya Mkazi wa Kata ya Makanyagio na AISHA SUNGURA (28) Mkazi wa mtaa wa Mji wa Zamani kwa tuhuma za shambulio la mwili.                                          Kamanda wa Polisi Katavi-Dhahiri Kidavashari

MAUAJI KATAVI

Image
Na.Issack Gerald- Katavi Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la   KAZIMIRI MASUMBUKO(49) MKAZI NA MKULIMA WA MISANGA aliuawa kwa kuchomwa kitu chenye ncha kali sehemu za mgongoni, mkononi, mkono wa kushoto na kidevuni na watu wasiofahamika                                                Kamanda wa polisi Katavi-Dhahiri Kidavashari

KIPINDUPINDU KATA YA KAWAJENSE KAMA CHOO HAITAJENGWA

Na.Agness Mnubi-MPANDA WAFANYABIASHARA wa soko la Majengo mapya kata ya Kawajense Manispaa ya Mpanda wanakabilwa na ukosefu wa huduma ya choo sokoni hapo, hali inayoweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu.

WATAHINIWA 5422 KATI YA 6378 DARASA LA SABA WAFAULU KUJIUNGA NA MASOMO YA SEKONDARI KATAVI 2016

MPANDA-Na.Meshack Ngumba JUMLA ya Watahiniwa 5,422 Kati ya watahiniwa 6,378 waliofanya mtihani wa kuhitimu elimu ya Msingi Mkoani Katavi wamefaulu Kujiunga na Kidato cha Kwanza Kwa Mwaka 2016.

VIKUNDI 14 VYA WAJASILIAMALI 60 MPANDA WAKOPESHWA MILIONI 27

Na.Agness Mnubi-MPANDA. WAJASIRIAMALI   60   sawa na   vikundi 14 kutoka Wilayani Mpanda na Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamepata mkopo wa sh. Million 27 kupitia Mfuko wa Wajasiriamali Mpanda(METF).

SERIKALI YA TANZANIA KUZIMA SIMU BANDIA IFIKAPO JUNI,2016

Image
Na.Katibu Mkuu Kiongozi-DAR ES SALAAM Katibu Mkuu kiongozi Omben Sefue kwa kushirikaana na mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA imetoa tamko rasmi kuwa simu zote   mkononi zisizo halali yaani Bandia zitafungwa kutmumika ifikapo mwezi juni mwaka 2016.                                                        

WATOTO 62 WENYE MAHITAJI MAALUMU WAIBULIWA MPANDA,WAMO ALBINO WAWILI WALIOPELEKWA SUMBAWANGA KUSOMA

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA Jumla ya watoto 62 wenye mahitaji maalumu wakiwemo wawili wenye ulemavu wa ngozi albino wamefichuliwa Wilayani Mpanda wakiwa katika mazingira yanayowanyima haki zao za msingi ikiwemo kupatiwa   elimu kwa kipindi cha mwezi Juni hadi Desemba mwaka huu.                                             Baadhi ya watoto wenye mahitaji maalumu Wilayani Mpanda.PICHA Na.Issacka Gerald

JESHI LA POLISI KATAVI LAANZA KUTOA TAHADHARI MSIMU WA SIKUKUU 2015

Na.Issack Gerald-Katavi Wakazi Katika Mkoa wa Katavi wametakiwa kuepukana na Mazingira hatarishi Katika kipindi hiki cha kuelekea Kipindi cha sikuku za Krismasi na mwaka mpya.

KAMATI ELIMU JUMUISHI MPANDA KUFANYA KIKAO LEO

Na.Issack Gerald-MPANDA Kamati ya kushughulikia elumu jumuishi Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,leo wanatarajia kukutana na wadau wa elimu hiyo kujadili masuala mbalimbali.

WAKAZI MPANDA WACHARUKA KUANDIKIWA RISITI TOFAUTI NA PESA WANAYOLIPA KWA USHURU WA KUZOA TAKA

Na.Issack Gerald-MPANDA BAADHI ya wakazi wa mtaa wa Mpanda Hotel   C Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wamelalamikia hatua ya kupewa lisiti iliyoandikwa fedha tofauti na kiasi wanacholipa kwa ajili ya kuzoa taka katika mtaa huo.

WANAWAKE MPANDA WATAKIWA KUJIFUNGULIA HOSPITALINI KUPAMBANA NA VIFO

Na.Vumilia Abel-MPANDA Wanawake Wilayani Mpanda Mkoani Katavi wametakiwa kuona umuhimu wa kujifungulia katika vituo vya afya na kuachana   mila potofu za kujifungulia nyumbani ili kuzuia voifo visivyo vya lazima.

DAMU SALAMA YAKUSANYWA MPANDA

Image
Na.Lutakilwa Lutobeka-MPANDA Wizara ya afya kupitia kitengo cha damu salama Wilayani Mpanda Mkoani Katavi kimewapongeza wananchi walojitokeza katika zoezi la uchangiaji wa damu huku kikiwaomba ambao hawajachangia wafanye hivyo ili kuokoa uhai wa wagonjwa.                                                            Damu salama iliyokusanywa

KESI YA KUBENEA DHIDI YA MAKONDA YAAHIRISHWA KUSIKILIZWA DESEMBA 29

Image
Na.Yusuph Katimba - Dar es Salaam KESI iliyofunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda dhidi ya Mbunge wa Ubungo, Said Kubenea katika Mahakama ya Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo, imeahirishwa.                                                   Said Kubenea Mbunge jimbo la Ubungo

UONGOZI CHADEMA KATAVI,JIMBO NA WILAYA WASIMAMISHWA UONGOZI.

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,kanda ya kusini Magharibi,umewasimamisha viongozi wa chama hicho kwa Mkoa wa Katavi,kwa jimbo la Mpanda na wilayani Mpanda,kwa tuhuma kukihujumu chama.                                                          Bendera ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema

TANROAD KATAVI WATAJA MIKAKATI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA KATAVI

Image
Na.Issack Gerald-MPANDA   WAKALA wa barabara Tanzania TANROADS Mkoani Katavi wamesema, wanafanya mchakato wa kupata wakandarasi wa kujenga miundombinu ya barabara zinazounganisha Mkoa wa Katavi na mikoa jirani.                                                    TANROADS

MTOTO ANAYEDAIWA KUUWAWA NA ASKARI KWA RISASI MLELE AZIKWA

Na.Issack Gerald-MPANDA Wazazi wakazi wa kijiji cha Kamsisi Wilayani Mlele Mkoani Katavi wamekubali kuuzika mwili wa mtoto wao Moshi Saleh (17) anayedaiwa kuuwawa kwa kupigwa risasi za moto na askari wa wanyama pori wa shirika la hifadhi za Taifa Tanapa Mkoani hapa.

HABARI PICHA DAR ILIVYOKUWA KILELE CHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATIRI JANA

Image

MADIWANI NSIMBO WATAKIWA KUSIMAMIA SHUGHULI ZA MAENDELEO

Na.Issack Gerald-NSIMBO Baraza la madiwani la halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi, limetakiwa kusimamia kikamilifu shughuli za maendeleo katika kata zao pamoja na kutunza siri za serikali.

ASKARI 38 WA WANYAMA PORI WATUNUKIWA VYETI KATAVI

Na.Issack Gerald-MPANDA Jumla ya wahitimu 38 walioshiriki mafunzo awamu ya pili ya Kijeshi katika Hifadhi ya Wanyama pori Katavi, wametunukiwa vyeti katika madaraja mbalimbali.

MADIWANI MPANDA WATAKIWA KUWAJIBIKA KWA WANANCHI

Na.Issack Gerald-MPANDA . MADIWANI wanaounda baraza la madiwani halmashauri wa wilaya ya mpanda walioapishwa leo wametakiwa kuanza kazi kwa kuzingatia maadili na kuacha kufuata itikadi ya vyama vyao ili kuleta maendeleo ya wananchi kwaujumla.

HAKI ZA BINADAMU WACHARUKA KUHUSU UKATIRI UNAOENDELEA MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald-Mpanda Wananchi Mkoani Katavi wametakiwa kuripoti matukio ya ukiukwaji   wa haki za binadamu katika Ofisi za haki za binadamu wanapoona mamlaka husika Mkoani hapa zinawanyanyasa katika haki zao mbalimbali.

WANAWAKE KATAVI WAASWA KUTOA TAARIFA ZA UKATIRI

Na.Issack Gerald-MPANDA . WANAWAKE Mkoani Katavi wametakiwa kutoa taarifa za vitendo vya ukatili vinavyojitokeza katika familia na jamii kwa ujumla.

SHULE BINAFSI MPANDA ZAOMBA RUZUKU KUENDESHA SHULE ZAO ILI KUTEKELEZA AGIZO LA SERIKALI

Na.Issack Gerald-MPANDA WASIMAMIZI   wa shule binafsi wameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa Kuzipatia ruzuku za Uendeshaji endapo agizo la ada elekezi lililotolewa na serikali litapitishwa.

WANANCHI MKOANI KATAVI WATAKIWA KUCHANGIA DAMU SALAMA

Na.Issack Gerald-MPANDA. WANANCHI Mkoani Katavi wametakiwa kujitokeza kwa hiari ili kuchangia damu Salama.

BREAKING NEWS : VIONGOZI CHADEMA WILAYANI MPANDA WABWAGA MANYANGA

Na.Issack Gerald-MPANDA . BAADHI ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Wilayani Mpanda Mkoani Katavi wamejiuzuru wadhifa wao kutokana na usaliti   ndani ya chama uliotokea   kipindi cha uchaguzi mkuu wa ubunge urais na madiwani Oktoba 25 mwaka huu.

KAYA 8537 KATAVI ZANUFAIKA NA MRADI WA TASAF

Image
  Baadhi ya wanufaika wa Mradi wa Tasaf Mkoani Katavi Na.Issack Gerald-MPANDA KAYA 8537 katika vijiji   80 kati vijiji 177 vilivyopo Mkoani Katavi zimenufaika na mpango wa kunusuru kaya maskini Mkoani Katavi.

VIJIJI 7 WILAYANI NSIMBO VYALIA NA MIUNDOMBINU MIBOVU YA BARABARA

Na.Issack Gerald-NSIMBO                                                                       ZAIDI ya vijiji saba katika Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo           Mkoani   Katavi vinakabiliwa na ubovu wa miundombinu ya barabara inayounganisha kijiji kimoja na kingine.

CHANAGAMOTO ZAENDELEA KUIANDAMA SHULE YA MSINGI KAWANZIGE

Na.Issack Gerald-MPANDA. SHULE ya Msingi Kawanzige iliyopo Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi yenye jumla ya wanafunzi 663 inakabiliwa na upungufu wa madarasa ya wanafunzi pamoja na ofisi za Walimu.

MKUU WA MKOA WA RUKWA AAGIZA KUOANDOLEWA MAAFISA WANNE KITENGO CHA FORODHA MKOANI HUMO

Image
Baadhi ya magogo yaliyokamatwa Na Mwandishi wetu- SUMBAWANGA. MKUU wa Mkoa wa Rukwa Magalula Ssaid Magula ameagiza kuondolewa mara moja kwa maofisa wa vitengo vinne kutoka katika kituo cha forodha cha Kasesya mpakani mwa nchi ya Zambia wilayani Kalambo mkoani humo kwa tuhuma za kushindwa kutekeleza maadili ya utumishi wa umma.

WANUFAIKA NA TASSAF WAPONGEZA MRADI HUO WILAYANI MLELE

Na.Issack Gerald-Mlele. BAADHI ya wakazi wa Ilunde na Isegenezya kata ya Inyonga wilayani Mlele Mkoani Katavi wameupongeza mradi wa kunusuru kaya masikini tasaf   kwa kuwawezesha kujikwamua kimaisha.

WAZAZI WATAKIWA KUHAKIKISHA WAANDIKISHA DARASA LA KWANZA WATOTO WAO

Na.Issack Gerald-MPANDA SERIKALI Imewataka Wazazi wote Kuhakikisha Watoto waliofikia Umri wa Kuanza Shule Kuandikishwa na Kuahidi kuwachukulia hatua watakaoshindwa Kutekeleza agizo hilo.

WASAFIRI MPANDA WALALAMIKA TRENI KUTOSAFIRISHA ABIRIA KWA MUDA MWAFAKA

Na.Issack Gerald-MPANDA Wasafiri wa treni mkoani katavi wamelalamikia suala la kukaa muda mrefu kwenye kituo cha treni kiasi kinachowafanya kushindwa kusafiri kwa wakati unaotakiwa.

WALEMAVU KATAVI WAOMBA MITAJI NA MIRADI YA MAENDELEO KUONDOKANA NA UMASKINI

Na.Issack Gerald-MPANDA Watu wenye ulemavu mbalimbali Mkoani Katavi wameiomba serikali ya Tanzania kuwapatia miradi ya maendeleo   pamoja na kujenga miundombinu rafiki kwao itakayowasaidia kupunguza ugumu   wa maisha.

WANAWAKE MPANDA NDOGO NA KABUNGU WAONGOZA KWA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI

Na.Issack Gerald-MPANDA Jumla ya watu 14 kati ya 169 waliopima Virusi vya Ukimwi Mwezi Novemba mwaka huu katika Kata ya Kabungu na Mpanda Ndogo wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.