Posts

Showing posts from March 31, 2018

JUMAMOSI KUU

Image
Jumamosi kuu  ni  siku  ya  Juma kuu  inayoadhimisha hasa  pumziko  la  mwili  wa  Yesu Kristo   kaburini  kabla ya  kufufuka  kwa  utukufu   usiku  wa kuamkia  Jumapili  ya  Pasaka . Tarehe  yake inabadilikabadilika kila  mwaka  na hata mwaka uleule ni tofauti katika  madhehebu  ya  Ukristo , hasa yanayofuata  mapokeo  ya  mashariki  na yale yanayofuata mapokeo ya  magharibi . Siku hiyo  Misa  na  sakramenti  mbalimbali haziadhimishwi kwa kuwa  wafuasi  wa  Yesu  wanatulia  kimya  wakitafakari matukio ya  Ijumaa kuu  na kujiandaa washangilie  ufufuko wake kuanzia  kesha  la Pasaka hadi  Jumapili  ya  Pentekoste  siku  50  baadaye. Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com