Posts

Showing posts from November 6, 2017

RAIS MUGABE AMEMTUMBUA JIPU MAKAMU WAKE WA RAIS

Image
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amemfuta kazi Makamu wake wa Rais Emmerson Mnangagwa. Emmerson Mnangagwa Kwa mjibu wa Waziri wa Habari wa Zimbabwe Simon Kahaya Moyo,Bw.Mnangagwa (75) ameachishwa kazi kwa madai kuwa alionyesha tabia za kukosa uzalendo na uaminifu hasa kwa Rais. Kufutwa kwake ni ishara kuwa mke wa rais Robert Muabe, Bi.Grace,atafuata nyayo za mumeme za kuwa rais wa Zimbabwe Siku ya Jumapili Bi.Grace Mugabe alitoa wito wa kutaka mumewe amfute kazi Mnangagwa. Bw.Mnangagwa ambaye ni mkuu wa zamani wa idara ya ujasusi,amekuwa kwenye mstari wa mbele kumrithi Rais Mugabe. Kufutwa kwake kunakuja baada ya Rais Robert Mugabe(93)kutishia kumuachisha kazi Bw Mnangagwa, hatua ambayo imezua uvumi kuwa anataka mke wake kuchukua hatamu za kuliongoza taifa hilo. Akihutubia mkutano wa wanachama wa makanisa ya asili mji Harare siku ya Jumapili,Bi Mugabe alisema Bw Mugabe alimtaka Mnangagwa na wafuasi wake kumuonyesha uzalendo au afutwe kazi. Chama cha Zanu-PF kinataraj

WATOTO 2 WAMEPOTEA KATIKA MAZINGIRA TATANISHI MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald WATOTO wawili wakazi wa kitongoji cha Mnyaki B Rama na Vitisho wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 9 na 11 Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,wamepotea katika mazingira ya kutatanisha. Mwenyekiti wa kitongoji cha Mnyaki B Bw.Alex Gezaho,amethibitisha kupotea kwa watoto hao Jumamosi iliyopita ambapo amesema,walikuwa wakiwinda ndege pori kwa manati. Kwa mjibu wa baadhi ya wakazi wa kitongoji cha Mnyaki B,watoto hao ambao ni wanafunzi wa shule ya Msingi Mnyaki mmoja akisoma darasa la pili na mwingine darasa la tatu ni miongoni mwa watoto watatu waliokuwa wakiwinda ndege siku ya juzi walipopotea. Watoto hao wawili wametajwa kuwa walikuwa wakiishi kwa mama mmoja anayeishi katika kitongoji cha Mnyaki B ambaye naye ametambulika kwa jina la mama Mwereza.                        Mwenyekiti wa kitongoji cha Mnyaki B amesema,tukio kama hilo lilitokea miaka mitano iliyopita katika kitongoji hicho ambapo mtoto wa kike alipotea katika mazingira ya kutatani

WATOZA USHURU PUNGUFU TA TANI 1 KUKIONA CHA MOTO,SERIKALI KUANZA KULIPA MISHAHARA YA WATUMISHI WA UMMA MWEZI HUU

Image
Na.Issack Gerald Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.John Magufuli ameviagiza vyombo vya ulinzi na Usalama nchini kuwakamata watumishi na watoza ushuru wote nchini watakamtomtoza ushuru mwananchi anayesafrisha mzigo usiozidi tani moja. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo wakati akihutubia wananchi mjini Bukoba Mkoani Kagera ambapo alikuwa na shughuli ya kuweka jiwe la msingi upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba. Katika hatua nyingine,Rais Magufuli amesema kuanzia mwezi huu serikali itaanza kulipa stahiki zote za wafanyakazi wa umma wanazoidai serikali ikiwemo malimbikizo ya mishahara ambapo zaidi ya shilingi bilioni 159 zimetengwa kwa ajili hiyo. Rais magufuli amefanya ziara mkoani Kagera kama mwendelezo wa ziara zake za kikazi katika maeneo mbalimbali hapa nchini ambapo wiki iliyopita alifanya ziara katika mikoa ya Mwanza na Geita na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo. Kwa mjibu wa rais Magufuli,keshokutwa atakwenda Nchini Uganda kwa ajili ya kwenda kuweka jiwe