WATOTO 2 WAMEPOTEA KATIKA MAZINGIRA TATANISHI MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald
WATOTO wawili wakazi wa kitongoji cha Mnyaki B Rama na Vitisho wanaokadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 9 na 11 Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,wamepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Mnyaki B Bw.Alex Gezaho,amethibitisha kupotea kwa watoto hao Jumamosi iliyopita ambapo amesema,walikuwa wakiwinda ndege pori kwa manati.
Kwa mjibu wa baadhi ya wakazi wa kitongoji cha Mnyaki B,watoto hao ambao ni wanafunzi wa shule ya Msingi Mnyaki mmoja akisoma darasa la pili na mwingine darasa la tatu ni miongoni mwa watoto watatu waliokuwa wakiwinda ndege siku ya juzi walipopotea.
Watoto hao wawili wametajwa kuwa walikuwa wakiishi kwa mama mmoja anayeishi katika kitongoji cha Mnyaki B ambaye naye ametambulika kwa jina la mama Mwereza.                       
Mwenyekiti wa kitongoji cha Mnyaki B amesema,tukio kama hilo lilitokea miaka mitano iliyopita katika kitongoji hicho ambapo mtoto wa kike alipotea katika mazingira ya kutatanisha na mpaka sasa hajapatikana.
Mbali na tukio hilo la kupotea kwa watoto,matukio mengine ambayo yamekuwea yakitokea katika kijiji cha Mnyaki kwa ujumla ni pamoja na matukio ya watu kuvamiwa usiku na kuporwa mali na fedha zao huku wengine wakijeruhiwa kutokana na silaha sinazotumiwa na waharifu.

                          Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA