Posts

Showing posts from June 11, 2018

MWANAMKE ASIYEJULIKANA ATUPA MTOTO WA UMRI WA SIKU 1 KATIKA UWANJA MICHEZO

Mtoto wa jinsia ya Kike anayekadiriwa kuwa na umri wa   siku 1 ameokotwa akiwa hai katika uwanja wa Azimio   Halmashauri ya manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi baada ya kutupwa   na mwanamke ambaye mpaka sasa hajafahamika majina wala makazi yake. Mashuhuda wa tukio wakilaani tukio hilo,wamesema mtoto huyo inasadikiwa alitupwa Ijumaa ya Juni 8 mwaka huu majira ya mchana mpaka alipookotwa majira ya saa kumi   jioni . Hata hivyo wananchi wilayani Mpanda wamesikitishwa na tukio hilo na kuomba   hatua kali zichukuliwe dhidi ya mwanamke atakayebainika kutenda unyama huo dhidi ya mtoto asiyekuwa na hatia. Kwa upande wake Afisa Ustawi wa jamii manispaa Redgunda Mayorwa amethibitisha kupokea taarifa za mtoto huyo ambapo amesema jeshi la polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kumpata na kumfikisha katika vyombo vya sheria mwanamke aliyetenda unyama huo. Aidha ametoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali na jeshi la Polisi kuhusiana na tukio hilo kwa kuwa ki