Posts

Showing posts from August 28, 2017

POLISI,JAJI MKUU WATOA ONYO MGOMO WA MAWAKILI HAPA NCHINI-Agosti 28,2017

Image
Kaimu  Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma na Jeshi la Polisi nchini,wamelionya Baraza la Uongozi la Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS),kutoingilia vyombo vya uchunguzi na upelelezi,vinavyochunguza tukio la mlipuko,uliotokea kwenye ofisi za Kampuni ya Mawakili ya IMMMA usiku wa kuamkia juzi jijini Dar es Salaam.

POLISI WAWEKA WAZI MAJIBU YA UCHUNGUZI OFISI ZA MAWAKILI IMMMA KULIPULIWA-Agosti 28,2017

Image
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, leo limesema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa watu wasiojulikana utambulisho wao na idadi yao walifika katika ofisi za Mawakili wa IMMMA Advocates wakiwa katika magari mawili na kujifanya ni maaskari na kuwarubuni walinzi na kuondoka nao katika gari mojawapo kabla ya kulipua jengo hilo.

RAIS MAGUFULI AWATAKA TAKUKURU KUTOKUWA NA KIGUGUMIZI DHIDI YA WAHUSIKA VITENDO VYA WA RUSHWA-Agosti 28,2017

Image
Rais Magufuli akiwa ndani ya Ofisi ya Takukulu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU ) kutokuwa na kigugumizi cha kuchukua hatua pale wanapokuwa na ushahidi dhidi ya watu wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.