MSITU WA TONGWE MAGHARIBI WENYE SOKWE ZAIDI YA 800 SASA MIKONONI MWA HALMASHAURI YA WILAYA YA MPANDA

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mbwana Muhando akizungumza na wananchi wa kijiji cha Katuma(PICHA NA Issack Gerald)
Sokwe moja ya wanyama wanaopatikana msitu wa Tongwe Magharibi
Baadhi ya wananchi katika kijiji cha Kapanga wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Mpanda Salehe Muhando(Hayupo pichani)(PICHA NA Issack Gerald)

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoani Katavi Salehe Muhando,amesema wizara ya maliasili na utalii imekubali msitu wa Tongwe Magharibi kumilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda kutoka katika mamlaka ya wizara hiyo.
Muhando amebainisha hatua hiyo kupitia mikutano ya hadhara katika vijiji vya Kapanga na Katuma Kata ya Katuma lengo likiwa ni kuelimisha kutunza msitu huo wenye zaidi ya sokwe 800 kwa ajili ya faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda Mh.Hamadi Mapengo amesema mchakato wa kuomba kumiliki msitu huo ulianza mwaka 2002 ambapo kwa sasa kutaongezeka mapatao yatokanayo na msitu ikiwa ni pamoja na kupata watalii kwa ajili ya kuja kuwaona wanyama.
Kwa mjibu wa Kaimu wa afisa ardhi na maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Bw.Elisha Mengele,vijiji vipatavyo 11 vinavyozunguka msitu huo vinatarajia kunufaika zaidi na msitu huo.
Amevitaja vijiji hivyo kuwa ni Lugonesi,Lwega, Kapanga, Katuma,Mpembe,Vikonge,Bugwe,Mlibasi,Isubangala na Kusi inayojumuisha vijiji vya Mishamo.
Hata hivyo kinachosubiriwa sasa ni msitu huo kutangazwa katika gazeti la serikali ili kumilikiwa rasmi na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda.
Katika ziara hiyo ambayo inafanyika katika vijiji vyote 11,mkuu wa wilaya alikuwa ameambatana pia na Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda,Mh.Theodora Romward Kisesa(Diwani Viti Maalumu ccm),Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi CCM Wilayani Tanganyika akiwa na Katibu wake Bw.Jackson huku pia mikutano hiyo ikihudhuriwa na wenyeviti wa vijiji,mabalozi na maafisa watendaji wa vijiji.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA