ANC CHAADHIMISHA MIAKA 100 YA KUZALIWA KWA NELSON MANDELA

Chama tawala cha Africa Kusini ANC kimeanza maadhimisho ya kumbukumbu za miaka mia moja tangu kuzaliwa kwa Raisi wa kwanza mweusi nchini humo shujaa Nelson mandela.
Nelson Mandela
Kiongozi wa sasa wa ANC ,Cyril Ramaphosa anatarajiwa kutoa hotuba huko medani mwa Freedom square mjini Cape Town, ambako marehemu Mandela alitoa hotuba yake ya kwanza alipoachilia huru kutoka gerezani miaka ishirini na nane iliyopita.
Rais Jacob Zuma ambae anakabiliwa na madai chungu nzima ya rushwa amegoma kubanduka huku shinikizo za kumtaka ajiuzulu zikizidi kumzonga .
ANC imetangaza mkutano maalum wa kamati yake kuu ya kitaifa utafanyika Jumatatu kujadili swala hilo.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA