WANAFUNZI KIDATO CHA NNE KATAVI WAMESEMA WATAFAULU MTIHANI

Na.Issack Gerald-Katavi

Baadhi ya watahiniwa wa mtihani wa kidato cha nne katika shule mbalimbali za manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wameeleza matumaini ya kufaulu mtihani wao ulioanza leo nchi nzima.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti,wanafunzi hao wakiwemo wa shule ya sekondari Mwangaza na Kashaulili wamesema maandalizi yao katika mtihani huo yako vizuri huku wakiwaomba wenzao kuondoa hofu ya mtihani.
Kwa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Mwangaza Mwl.Simoni Lubange amewataka wanafunzi wake kujiamini na kumtanguliza mungu katika ujibuji wa mitihani yao kwa alichokisema hakuna kitu kigeni watakachokutana nacho.
Jumla ya watahiniwa 385,938 wa kidato cha nne nchini wameanza mtihani leo huku baraza la mitihani likitoa onyo kwa na tahadhari kwa wamiliki wa shule watakaofanya udanganyifu.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA