WAKAZI WILAYANI MPANDA WALALAMIKIA UBOVU WA MIUNDOMBINU YA RELI

Wananchi wilayani Mpanda  mkoani Katavi wamelalamikia shirika la reli kwa kutorekebisha miundombinu ya reli kwa wakati  katika eneo la Ugala mpaka Rumbe.

Wananchi hao wameeleza kuwa kumekua na ajali nyingi zikitokea kutokana na miundombinu ya eneo hilo kutokuwa salama kwa usafiri hali inayosababisha kupotea kwa mizigo.

Mkuu wa kituo cha reli  Mpanda  Bw.Vivian Lyapembile amesema kuwa pamoja na changamoto wanazopata  kwa sasa  ila wana ufahamu na  tatizo hilo na tayari wameanza mchakato wa kukarabati eneo hilo.

Hivi karibuni kumekuwa na changamoto ya usafiri kwa wasafiri wanaotumia usafiri wa treni hali inayosababishwa uchakavu wa miundo mbinu kwa baadhi ya maeneo pamoja na maeneo mengine reli kusombwa maji ya mvua zinazoendelea kunyesha. 


Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA