MKOANI WA RUKWA WAZINDUA KAMPENI YA UPANDANI MITI

MKOA wa  Rukwa umezindua kampeni ya upandaji miche ya miti kwa lengo la kuhifadhi mazingira ambapo katika kipindi cha mwaka huu unatarajia kupanda jumla ya  miche milioni sita katika halmashauri zote nne za mkoa huo.
Akizundua kampeni katika halmashauri ya wilaya ya Kalambo katika mji wa Matai,mkuu wa mkoa huo Joachim Wamgabo alisema kila halmashauri italazimika kupanda miche isiyopungua milioni 1.5 ambapo mpaka sasa tayari mkoa mzima umeotesha miche milioni 2,173,649 sawa na asilimia 36 ya miche itakayo pandwa.
Alisema yeye  amezindua kampeni hiyo kinachofuata ni watendaji wa serikali kuhakikisha wanasimamia na kutekeleza na ambapo itakapofikia mwishoni mwa mwaka halmashauri ambayo haitafikia lengo itatozwa faini ya shilingi milioni moja na fedha hizo itakabidhiwa halmashauri ambayo imetekeleza kampeni hiyo kwa asilimia mia moja.
Awali kabla ya kuzindua kampeni hiyo Wangabo alimuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kalambo Simon Ngagani amwajibishe Afisa mtendaji wa kiji cha Matai Ester Mwashambwa kwa kitendo cha kushindwa kuwahamasisha wananchi wajitokeze katika uzinduzi wa kampeni hiyo kwani waliofika walikuwa ni wanafunzi wa shule ya sekondari Matai na watumishi wa serikali.
Alisema wananchi ni wadau wakubwa katika suala la uhifadhi mazingira na ndiyo wakataji miti wakubwa kwa lengo la kupata nishati ya mkaa na kuni lakini kitu cha ajabu hawakuwepo katika uzinduzi huo hali iliyomkera mkuu huyo wa mkoa.
Naye mwakilishi wa wakala wa misitu Tanzania TFS wilayani Kalambo Herman Ndanzi alisema wakala huo una jumla ya hekta 1192 ambazo unazihudumia licha ya kuwa bado jitihada zinafanyika za kupanda miti ili kuongeza misitu.
Alisema wakala huo umewapatia wananchi kilogramu 6 za mbegu za miti ya aina tofauti ili wakaipande ambapo itasaidia kuhifadhi mazingira na kuwa inaendelea na suala kuwaelimisha wananchi waache kuharibu misitu.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA