KASI YA KUMNASUA MTOTO WA KIKE HASA MIMBA ZA UTOTONI YAZIDI KUSHIKA KASI

Na.Issack Gerald
WATOTO wa kike mkoani Rukwa wamepewa mafunzo maalumu ya namna ya kuzitambua changamoto mbalimbali zinazowakwamisha kuzitumia fursa zilizopo katika kutekeleza matarajio yao ili waweze kujitegemea.
Akizungumza katika uzinduzi wa mradi uitwao U-report unaotekelezwa na Tanzania Girl Guides Association mkufunzi wa mradi huo,Emiliana Stanslaus amesema wahitimu wapatao 20 katika kila halmashauri wamewezeshwa namna ya kuwasaidia wasichana wenzao katika kukabiliana na vitendo vya ukatili dhidi yao.
Amesema wasichana hao walipata mafunzo ya siku mbili ambapo watawasaidia wanafunzi wenzao wa kike katika shule za msingi na sekondari na wasichana waliopo vijijini katika kukabiliana na changamoto mbalimbali katika maisha yao ikiwa ni pamoja na kubakwa na pia kupata mimba za utotoni.
Emiliana amesema mradi huo utatekelezwa katika halmashauri za Sumbawanga vijijini,Kalambo,Nkasi na Sumbawanga Manispaa kwa njia ya kutuma ujumbe wa maandishi ya simu kwenda namba maalumu ya 15070 kwa mitandao yote na kunawawezesha walengwa kutoa taarifa kwenye vyombo na mamlaka zinazohusika dhidi ya vitendo vya ukatili walivyofanyiwa wasichana hao.
Tanzania Girl Guides Association kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na watoto ulimwenguni UNICEF-inatarajia kutoa mafunzo kwa wasichana zaidi ya 15 elfu watakaosaidia kuwaelimisha wenzao katika mikoa ya hapa nchini namna ya kukabiliana na vitendo vya ukatili.
Kwa upande wake Honorotha Wamai ambaye ni mkufunzi wa Girl Guides mkoani Rukwa amesema wasichana hao waliohitimu wanatakiwa kutoa mafunzo yanayohusu mradi huo katika halmasahuri zao za wilaya kwa kushirikiana na idara za elimu na maendeleo ya jamiii.
Awali akizindua mradi huo kwa niaba ya katibu tawala mkoa wa Rukwa,mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga John Msemakweli amesema serikali imetunga sheria zinazowalinda wasichana dhidi ya vitendo vya ukatili.
Amesema katika utekelezaji wa sheria hizo,serikali mkoani Rukwa itawafikisha mahakamani wazazi ambao watoto wao wanapata ujauzito pindi itakapobainika kuwa wameshiriki kuficha ukweli au vielelezo vitakavyosaidia kuwatia hatiani watuhumiwa wa kuwapa mimba mwanafunzi.
Habari zaidi na P5TANZANIA LIMITED
Top of Form

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA