ACT-WAZALENDO WAINGILIA KATI MIGOGORO YA ARDHI KATAVI


Viongozi wa Mkoa wa chama cha ACT-Wazalendo wakiwa na viongozi wa kata ya Sitalike,wamefika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga kwa ajili ya kutafuta mwafaka wa mashamba na mazao ya wananchi katika kata hiyo.
Mwenyekiti wa chama hicho Bw.John Malack akiwa na Katibu wake Bw.Joseph Mona Mkuu wa Mkoa wakizungumzia hatua hiyo jana mara baada ya kutoka katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wamesema wamefikia hatua hiyo kama sehemu ya kusimamia maslahi ya wananchi kwa kuwa ni wajibu.

Aidha wamesema wataendelea kufanya hivyo na kutafuta tafsiri za kisheria kuhusu migogoro ya ardhi inayoendelea katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Katavi.
Baadhi ya wananchi wa kata hiyo ambao wameambatana na ujumbe wa ACT-Wazalendo pamoja na mambo mengine wamesema wameridhishwa na majibu ya Mkuu wa Mkoa  huku mwenyekiti wa kijiji cha Sitalike Bw.Christopher Mrisho akisema wananchi wapatao 3500 wa vitongoji vya situbwike,Makutanio na Mgorokani wameathiriwa zaidi.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga amekiri kuwaruhusu wakazi walioondolewa katika makazi yao kuvuna mazao yao huku akisema atapanga ratiba ya kwenda kufanya Mkutano wa hadhara ili kuzungumza na wananchi.
Hata hivyo baadhi ya wananchi wameendelea kukosa sehemu ya kujenga makazi na kuendesha shghuli za kilimo licha ya serikali kusema imetenga hekari zaidi ya 7000 kwa ajili ya wakazi hao ambapo kwa upande wa wananchi bado wanadai hawajaelekezwa hekari hizo zinakopatikana.
Oparesheni ya kuwaondoa wakazi hao wanaodaiwa kuvamia maeneo ya hifadhi ilifanyika Mwezi Agosti mwaka 2017.
P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA