RAIS MAGUFULI AWAONYA TRA


Rais Dkt.John Magufuli amemuagiza Kamishna wa TRA,Waziri wa Fedha na katibu mkuu kwenda kuishughulikia Shirika la Mapato Tanzania (TRA) ili iweze kuacha tabia zake chafu za kuwaongezea raia kodi za mapato pindi wanapokwenda kupata huduma hizo.
Dkt.Magufuli ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa anatoa hotuba yake kabla ya kuweka jiwe la msingi wa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa ya 'Standard Gauge' katika eneo la Ihumwa,Dodoma ambapo awamu ya kwanza ilizinduliwa mwezi Aprili mwaka 2017,katika maeneo ya PUGU, Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na hayo,Dkt. Magufuli ameendelea kwa kusema "TRA muangalie kodi zenu mnazozitoza, inawezekana nyingine ni kubwa mno kuliko miradi wanayotekeleza wananchi badala ya kuwa motisha kwa walipa kodi inakuwa kero kwao na badala yake wanabuni njia ya kukwepa kulipa kodi.
Kwa upande mwingine,Dkt. Magufuli ameitaka TRA kuendelea kutoa elimu ya mlipa mkodi kwa wananchi ili kuweza kuwapa uelewa wanachi na waweze kulipa kodi kwa heshima kwa taifa lake.
Habari zaidi ni P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA