BAVICHA WATOA NENO KWA SERIKALI KUHUSU AMANI NCHINI



Baraza la vijana la Chadema (Bavicha) Mkoani Rukwa limeitaka Serikali kutumia gharama yoyote kulinda amani ya nchi inayoonesha dalili ya kutoweka kutokana na kukithiri kwa vitendo vya mauaji ya kinyama na utekaji unaofanywa watu wasiojulikana.
Makamu Mwenyekiti wa Bavicha,John Pambalu alisema hayo juzi wakati wa akifungua kongamano la vijana lilolenga kuwapa elimu wanachama wake  kuhusu wajibu wao katika siasa za sasa ambalo liliandaliwa na Bavicha mkoa wa Rukwa.
Alisema hali ya kisiasa hivi sasa hapa nchini ni tete kutokana kushamiri kwa vitendo vya utekaji na mauaji ya kinyama yanayofanywa na watu wanaodaiwa kutojulikana huku serikali ikiwa haijavalia njuga vya kutosha katika kudhibiti vitendo hivyo.
Makamu huyo mwenyekiti alisema imefika wakati sasa serikali kutumia gharama yoyote ili kulinda amani ya taifa hili iliyoasisiwa na Baba wa taifa Mwl.Julius Nyerere ambaye katika utawala wake na zile zilizopita hawakukubali kuona amani ikitiwa doa.
Awali,Mwenyekiti wa Bavicha mkoa wa Rukwa,Aida Khenan aliwataka vijana wa Chadema mkoani humo kulitumia kongamano hilo kujifunza namna ya kukabiliana na changamoto za kisiasa ambazo zimekuwa zikiathiri ustawi wa vyama vya upinzani hapa nchini.
Khenan ambaye pia mbunge wa viti maalumu mkoani Rukwa,alisema vijana hao wanapaswa kutumia fursa ya kongamano hilo kubaini mbinu mbalimbali za kujiongezea kipato ili wajikwamue kiuchumia na hatimaye kuondokana na umasikini.
Wakati huo huo amesema ili vijana washiriki kikamilifu katika siasa za mageuzi wanapaswa wawe na nguvu ya kiuchumi hivyo makongamano kama hayo yanawapa fursa ya kubaini mbinu mbalimbali za kujiongezea kipato.
Habari zadi ni P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA