WANAFUNZI 22 WA SHULE YA SEKONDARI MIRAMBO MKOANI TABORA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUFANYA VURUGU-Agosti 19,2017

JUMLA ya wanafunzi 22 wa shule ya sekondari Mirambo Mkoani Tabora,wamefikishwa na kusomewa mashtaka 12 yanayowakabili ikiwemo kufanya vurugu katika kata ya Chemchemi.

Mwanafunzi mmoja kati ya hao imelazimika afuatwe Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora Kitete na kusomewa mashataka hayo licha ya kuwa alikuwa amelazwa akipatiwa matibabu kutokana na majeraha aliyoyapata katika vurugu hizo zilizotokea wiki iliyopita.
Akisoma mashtaka hayo mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Tabora Emanuel Ngigwana,wakili wa serikali Idd Mgeni ameieleza mahakama kuwa, watuhumiwa wote 22 wanadaiwa kufanya vurugu kwa kuwajeruhi wananchi na kuharibu mali zao.
Aidha Wakili mgeni amesema,Agosti 14 mwaka huu majira ya usiku wanafunzi hao wanadaiwa kuwajeruhi wananchi sita kwa kuwakata na vitu vyenye nchi kali ikiwemo mapanga na fyekeo ambapo amesema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Hata hivyo watuhumiwa wote 22 wamekana kuhusika na wamerudishwa mahabusu baada ya kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana ambapo ni mwanafunzi mmoja amepata dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wenye bondi ya shilingi milioni mbili kila mmoja na kesi hiyo itatajwa tena Agosti 31 mwaka huu.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA