MGOGORO WA ARDHI MTAA WA NSEMULWA BADO MBICHI,MKURUGENZI ATOA JIBU BILA SULUHU


NA.Issack Gerald-Katavi
Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imesema haijapokea malalamiko ya wakazi wa mtaa wa Nsemulwa kutopimiwa viwanja vyao na kutozwa kiwango kikubwa cha pesa tofauti na kilichopangwa kupitia mikutano.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji Manispaa ya Mpanda Bw.Suleiman Lukanga wakati akizungumza na Mpanda Radio ili kujibu suala la mgogoro wa ardhi uliopo Mtaa wa Nsemulwa kati ya Ofisi ya ardhi ya manispaa hiyo na wakazi wa mtaa huo.
Amesema kuwa viwanja vimekwishapimwa ambapo majibu haya yanakinzana na madai ya wakazi hao wanaohitaji kupimiwa viwanja.
Mgogoro wa viwanja kutopimwa na kutozwa kiwango kikubwa cha pesa kwa wakazi wa mtaa wa Nsemulwa, limedumu kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo bila kupatiwa ufumbuzi wa kudumu huku wakazi hao wakishindwa kufanya shughuli za maendeleo.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA