AACHIWA MKE KWA LAKI 8 BAADA YA KUFUMANIWA


MKAZIwa kijiji cha Ntumba kilichpo wilayani Tanganyika katika mkoa wa Katavi,Charles Sabuni (37)  amepwa  viboko 30 hadharani baada ya kushikwa ugoni na mke wa jirani yake Ntema Mwiwela,juzi usiku wa manane kijijini hapo.
Kwa mujibu wa Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa adhabu hiyo  alipewa mgoni huyo ili iwefundisho kwake na  kwa wanaume wengine wenye tabia kama hiyo.
Akisimulia tukio hilo mwenyekiti wa Kitongoji cha Ntumba Samwel Mbuya alisema lilitokea saa tisa usiku, juzi nyumbani kwa Mwiwela ambaye anaishi jirani na Sabuni.
Akifafanua alisema kuwa mchana wa siku hiyo ya tukio hilo Mwiwela alimuaga mkewe kuwa ana safiri ambapo alirejea nyumbani kwake ghfla usiku wa manane na kumkuta Sabuni akiwa amelala chumbani kwake.
“Mwenye mke alimthibiti mgoni wake huyo asitoroke huku akimwamuru apige mayowe huku akisema anaomba msaada kwani amefumaniwa na mke wa mtu ….. kele hizo ziliwaamsha wanakijiji wenzake ambao walikimbilia eneo la tukio na  walipigwa na kutwaa kumkuta Sabuni akiwa chumbani chini ya ulinzi wa Mwiwela “ alieleza.
Alieleza kuwa wananchi hao walielezwa na Mwiwela  kitendo alichofanyiwa na jirani yake Sabuni ambapo walipandwa na hasira na kuamuru aendelee kuwa chini ya ulinzi hadi kutakapopambazuka .
Inadaiwa kulipokucha wananchi hao wenye hasira walimuaru mwenzao huyo apewe adhabu kali ya kucharazwa viboko hadharani ili iwe fundisho kwake na kwa wanaume wengine wenye tabia kama hiyo
Hata hivyo Sabuni alinusurika baada ya viongozi wa kitongoji wakiongozwa na mwenyekiti Mbuya na kuwazuia wasimcharaze viboko hadharani  kwa kuwa watakuwa wamekiuka haki za binadamu .
Ndipo kilipoitishwa kikao cha dharura kikiwajumuisha viongozi wa serikali wa kitongoji hicho, wazee  pamoja na Mwiwela na ‘mgoni wake ambapo baada ya majadiliano marefu Sabuni alikubali kumlipa faini faini ya  kiasi  cha Shilingi 800,000/- ikiwa ni fedha alizotoa mahali wakati muoa mke wake .
Kwa mujibu wa Mbuya mara tu Mwiwela alipokabidhiwa kiasi hicho cha fedha hapo hapo alimkabidhi mke wake kwa Sabuni akidai kuwa hawezi kuendelea  kuishi naye kwa sababu sio muaminifu.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA