RAIS UHURU KENYATTA ASEMA HAKUBALIANI NA MAAMUZI YA MAHAKAMA HUKU WILLIUM RUTO NAYE AKITAKA TUME YA UCHAGUZI KUTANGAZA TAREHE MPYA YA UCHAGUZI-Septemba 2,2017


Naibu wa rais wa Kenya William Ruto

NAIBU rais wa Kenya,William Ruto,ameitaka tume ya uchaguzi ya Kenya kutaja rasmi siku ya kurudiwa kwa uchaguzi wa urais nchini humo.
Hatua ni baada ya Ijumaa mahakama ya juu zaidi kubatilisha ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta wa uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita,ikisema kulikuwa na dosari kubwa zilizokiuka katiba ya Kenya.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga aliyeusifu uamuzi huo wa mahakama,papo hapo alishutumu vikali tume ya uchaguzi ya Kenya IEBC na pia kuwalaumu waangalizi wa kumataifa kwa kile alichokitaja ' kuhalalisha udanganyifu uliotokea na kutaka uchunguzi zaidi ufanyike.
Amewataka waliohusishwa na udanganyifu huo kujiuzulu , kufutwa kazi na hata kuchukuliwa hatua za kisheria wakisema kamwe hawawezi kuaminiwa kusimamia uchaguzi ujao.
Rais uhuru Kenyatta akiwahutubia wafuasi wake jijini Nairobi. Alisema kuwa majaji waliobatilisha uchaguzi wkeni ni wakora
Kwa upande wake Rais Uhuru Kenyatta amesema japo anauhesimu hakubaliani na uamuzi huo uliofutilia mbali ushindi wake na kwamba yuko tayari kwa marudio ya uchaguzi huo unaotakiwa kufanyika katika kipindi cha miezi miwili ijayo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA