JESHI LA POLISI RUKWA:VIONGOZI WA DINI UOMBEENI MKOA WA RUKWA MAUAJI YAPUNGUWE



Na.Issack Gerald
JESHI la polisi mkoani Rukwa limewaomba viongozi wa dini wazidi kumuomba Mungu ili lifanikiwe kumaliza vitendo vya mauaji ya nayotokana na imani za kishirikina mkoni humo.
Kamanda wa polisi mkoani humo George Kyando ametoa ombi hilo kwa uongozi wa kanisa la Pool Of Siloam wakati akipokea msaada wa matairi Saba ya magari yaliyotolewa na kanisa hilo kwa lengo la kulisaidia jeshi hilo kukabiliana na uhaba wa vitendea kazi. 
Amesema kuwa miongoni mwa changamoto zinazoukabili mkoa wa Rukwa ni mauaji yanayotokana na imani za kishirikiana hivyo amewaomba viongozi wa dini kuuombea mkoa huo ili mauaji hayo yaishe. 
Kamanda Kyando amesema jitihada zimefanyika za kutosha katika kukabiliana na kumaliza vitendo vya uhalifu lakini changamoto iliyopo ni mauaji yanayotokana na imani Za Kishirikiana.
Katika hatua nyingine amesema jamii bila kumtegemea mwenyezi Mungu ni ngumu kuacha matendo maovu hivyo taasisi za dini zina jukumu hilo na iwapo wakiamua inawezekana kabisa binaadamu wanaishi kwa amani bila kutendeana matendo mabaya. 
Kwa upande wake kiongozi wa kanda ya Magaribi wa kanisa hilo mchungaji Wisdom Shangwe amesema wametoa Msaada wa matairi hayo yenye thamani ya shilingi 2,100,000 ili kulisaidia jeshi la katika kutekeleza majukumu yake. 
Amesema hivi sasa lengo  la kanisa hilo ni kusaidiana na serikali katika kuwasaidia vijana waachane na maovu pia waache kutumiwa na baadhi ya wanasiasa wasio na nia njema ambao wamekuwa wakiwatumia vijana kwa maslahi yao binafsi. 
Wakati huo huo,ameahidi kuendelea kuuombea mkoa wa Rukwa pamoja na taifa kwa ujumla sambamba na viongozi wa serikali ili waendelee kumtumainia mwenyezi Mungu wakati wanapotekeleza majukumu yao.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA