HOFU JUU YA EBOLA YATANDA MKOANI RUKWA-Agosti 26,2017

Kirusi cha Ebola
WAKAZI mkoani Rukwa wametakiwa kuondoa hofu kutokana na kuwepo kwa taarifa juu ya uwepo wa ugonjwa wa ebola baada ya mgonjwa mmoja kulazwa na kuendelea kupatiwa matibabu Katika hospital ya mkoa ya Sumbawanga anaeugua ugonjwa wenye dalili kama za homa ya Ebola.

Kaimumganga mkuu wa hospitali ya mkoa wa Rukwa Dkt Emmanuel Mtika alisema kuwa mpaka sasa bado haijathibitika kuwa mgonjwa huyo anaumwa ebola. 
Alisema kuwa Katika hospitali hiyo alipokelewa mgonjwa na kuanza kupatiwa matibabu na akaanza kutoka damu puani,mdomoni na kuharisha damu dalili ambazo anakuanazo pia mgonjwa wa ebola hali iliyozua hofu.
Baada ya hali hiyo walichukua vipimo na tayari wamevipeleka mabara kuu ya serikali jijini Dar es Saalam kwaajili ya uchunguzi na majibu yatatoka baada ya masaa 48 ndiyo ambayo yatatoa mwelekeo ya nini mgojwa huyo anaumwa. 
Kaimu mganga mkuu huyo alisema kuwa mpaka sasa haiwezekani kutamka kuwa kuna homa ya Ebola mpaka hapo majibu yatakapo  tolewa kwani magonjwa ambayo yanadalili kama hizo nimengi lakini alitoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari. 
Alisema tayari idara ya afya imekwisha chukua hatua ikiwemo nipamoja na kwenda nyumbani alipotokea mgonjwa huyo ili kuweka tahadhari kwani nivizuri kuchukua tahadhari kabla ya hatari. 
Hata hivyo hofu na mashaka imewakumba wakazi wa wilaya ya kalambo hususani kijiji cha Kasanga alipotokea mgonjwa huyo kuwa tayari ugonjwa wa ebola umeshafika Katika kijiji chao. 
Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho Peter Simzosha alisema kuwa kutokana na kuzagaa kwa taarifa hizo baadhi ya wananchi wanafikilia kukikimbia kijiji hicho wasijekupata ugonjwa huo hatari.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA