SHIRIKA LA INTERNATIONAL AID SERVICES LATOA MSAADA WA MAFUTA KWA AJILI YA WENYE ULEMAVU WA NGOZI-Agosti 8,2017



SHIRIKA la International Aid Services(IAS) limetoa msaada wa mafuta yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi Albino ili kuzuia mionzi mikali ya jua inayochoma ngozi zao.

Akizungumza jana kupitia kikao baina ya shirikia hilo na kikundi cha walemavu na wazazi wa watoto wenye ulemavu, Mkurugenzi wa shirika la IAS linalojishghulisha na kutoa msaada kwa watu wenye ulemavu katika mikoa ya Rukwa na Katavi Bi.Irene Shayo,amewataka watu wenye ulemavu kushirikana katika matatizo pamoja na kutoa sauti ya pamoja kuhusu na matatizo yanayowakabili.
Lakini pamoja na mambo mengine Irene Shayo ameelezea jinsi shirika linavyofanya kazi ya kuibu watoto wenye ulemavu katika mikoa miwili pekee Tanzania ya Katavi na Rukwa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa shirika la IAS hapa nchni Bw.Jacksom Kaluzi amesema pamoja na shirika la International Aid Services kuchangia shilingi laki moja katika mfuko wa kikundi cha walemavu na wazazi wa watoto wenye ulemavu,amekitaka kikundi hicho kuibua miradi ya maendeleo itakayowasaidia kujiendeleza baada ya shirika hilo kujiondoa katika ufadhili.
Akizungumza kwa niaba ya wanachama 46 wa kikundi cha walemavu na wazazi wa watoto wenye ulemavu,mwenyekiti wa kikundi hicho Bernard Nkana ambaye pia ni mwenyelkiti wa mtaa wa Mpadeco Kata ya Makanyagio Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,amesema kwa upande wao kama wanachama wanakusudia kuanzisha miradi ya maendeleo kwa ajili ya kusaidia watoto wenye ulemavu ili wakamilishe ndoto zao.
Baadhi ya wazazi wenye watoto wenye ulemavu wamesema wanapata shida sana katika malezi hasa wanapokosa vifaa saidizi kwa watoto wenye ulemavu.
Wakati huo Shirika limesema linaendelea na mchakato wa kushughulikia baiskeli kwa ajili ya baadhi watu wenye ulemavu pamoja na kushirikiana na serikali katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayowaguza watoto wanaohitaji kupatiwa elimu kama watoto wasiokuwa na ulemavu.
Shirika la International Aid Services(IAS) linashirikiana na mashirika mengine ya Free Pentecostal Church Of Tanzania(FPCT) na International Centre Of Disabilities(ICD) ambayo kwa pamoja yanaunda umoja uitwao IFI

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA