MADEREVA BAJAJI WILAYANI MPANDA MKOANI KATAVI WAGOMA,SUMATRA WATOA TAMKO KALI WASISITIZA HAKUNA BAJAJI KUPITA BARABARA KUU KUANZIA KESHO AGOSTI 8,2017



WAENDESHA pikipiki za tairi tatu maarufu kama bajaji Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,leo wamegoma kutoa huduma ya usafiri wakilalamikia hatua ya Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi kavu SUMATRA kuwazuia kutumia barabara kuu zinazotoka mpanda mjini na kusafirisha abiria kupitia barabara kuu.
 

Akizungumza na waandishi wa habari mbele ya mamia ya waenedsha bajaji  kwa niaba ya waendesha bajaji Mkoani Katavi,Bw.Rashid Juma amesema,mipaka ya usafirishaji abiria ambayo imewekwa na Sumatra inawadidimiza kiuchumi kwa kuwa wanategemea kuendesha maisha ya familia zao kutokana na vyombo hivyo vya usafiri.
Kwa upande wake Afisa wa mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa majini na nchi Kavu Sumatra Mkoani Katavi Bw.Aman Mwakalebela amesema kuanzia kesho Agosti 8 hakuna pikipiki aina ya bajaji itakayoruhusiwa kutumia barabara hususani kutoka Mpanda mjini kupitia barabara ya Sumbawanga na Kigoma.
Hata hivyo Naye mwenyekiti wa usafirishaji Mkoani Katavi Nassoro Alfi ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani Mkoani Katavi amekiri kupokea taarifa ya mgomo ambapo ameshauri  serikali itumie busara katika suala hilo kutokana na kutokuwepo njia nyingine mbadala zitakazomwezesha dereva wa babajaji kupita kumfikisha abiria mahali anatkotakiwa kufika.
Katika hatua nyingine kutokana na mgomo wa madereva bajaji,baadhi ya wagonjwa,wajawazito wameshindwa kufika katika vituo vya afya ambapo pia abiria na madereva wa bajaji wameelezea kuathiriwa na mgomo huo.
Habarika zaidi na www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA