SUMATRA KATAVI YATOA MIEZI 3 KWA BODABODA KUKATA LESENI-Agosti 16,2017

Mamlaka ya uthibiti na usafiri wa nchikavu na  majini mkoani   katavi umetoa muda wa miezi mitatu kwa waendesha pikipiki maarufu kama boda boda  katika halmashauri ya wilaya ya mlele wawe wamekamilisha ukataji wa lesen za vyombo vyao vya moto pamoja na lesen za udereva.

Agizo hilo limetololewa leo na meneja wa SUMATRA mkoani  Katavi Bw.Aman mwakalebela wakati akitoa semina elekezi kwa waendesha boda boda hao katka halmashauri hiyo.
Amesema imekuwa ni kawaida kwa waendesha pikipiki hao kuendesha pasipo kuwa na lesen kutoka SUMATRA pamoja na kutokuwa na leseni za udereva.

Katika hatua nyingine ametoa onyo kwa wapiga debe na mawakala wa mabas katika stend ya mabasi Inyonga kwa kupandisha nauli kiholela pasipo kufuata mwongozo wa Mamlaka ya uthibiti na usafiri wa nchi kavu na  majini SUMATRA.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA