MADAI YA WAKAZI WA KITONGOJI CHA MGOLOKANI MKOANI KATAVI KUDAI KUWAMIWA NA SERIKALI NA KUBOMOLEWA MAKAZI YAO WAKATI WA OPARESHENI YA KUWAONDOA WAVAMIZI WA HIFADHI ZA MISITU KUWAKUTANISHA VIONGOZI WA WILAYA YA MPANDA KUSAKA SULUHU-Agosti 15,2017



HALMASHAURI ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi ijumaa ya wiki hii,inatarajia kukutana na Uongozi wa Wilaya ya Mpanda pamoja na viongozi wa hifadhi ya misitu Wilayani Mpanda, kujadili madai ya wananchi wa kitongoji cha Mgolokani kilichopo kijiji cha Matandalani kata ya Sitalike halmashauri ya Nsimbo wanaodai kuvamiwa na Serikali na kuharibu makazi yao kwa madai yanayotolewa na serikali kuwa wakazi hao wamejenga makazi yao katika eneo la hifadhi ya misitu.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mh.Raphael Kalinga amebainisha hayo leo wakati akieleza hatua zinazochukuliwa na Halmashauri ili kutafuta ufumbuzi wa madai ya wakazi wa kitongoji cha Mgolokani wanaodai pia kuwa wapo nje ya mipaka ya hifadhi ambapo mpaka sasa mamia ya wakazi kwa zaidi ya wiki moja tangu kubomolewa makazi yao wameendelea kuishi chini ya miti.
Wiki iliyopita,mwenyekiti wa kitongoji cha Mgolokani Bw.Divason Kisulo alisema mpaka sasa kaya zipatazo 215 zimebomolewa makazi ya yao na baadhi ya mali zao zikiwemo sola za umeme kupotea wakati wa zoezi la ubomoaji ambapo wakazi wapatao zaidi ya 1075 wanatarajia kuathirika ikiwa oparesheni katika eneo hilo litaendelea.
Wakati huo huo wakazi wa eneo hilo walidai mtu mmoja alifariki dunia kwa kugongwa na gari na mwingine kujeruhiwa kwa kile ambacho wananchi walidai kuwa walipatwa na ajaili hiyo katika harakati za kubomoa makazi yao.
Wakazi wa kitongoji cha Mgolokani wanadi kuishi katika kitongoji hicho kuanzia mwaka 1974 ambapo mwezi Julai mwaka huu 2017 wahifadhi wa misitu walifika kuhakiki mipaka na wakazi hao kuhakikishiwa kuwa wao wako eneo salama hali ambayo iliwaacha na mshangao nyumba zao zilipoanza kubomolewa.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Bi.Lilian Charles Matinga amekuwa akisisitiza kuwa lazima waliojenga ndani ya hifadhi katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya Mpanda lazima watii agizo la kuondoka katika maeneo hayo.
Maeneo mengine ambayo yamekumbwa na oparesheni ya kuwaondoa wakazi wanaodaiwa kuvamia hifadhi za misitu hivi karibuni ni kijiji cha Litapunga pamoja na Kitongoji cha Makutanio katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.
Habari zaidi Bofya www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA