CHAMA CHA ACT WAZALENDO CHALAANI UCHOMAJI MOTO MAKAZI YA WATU KATAVI-Agosti 25,2017

CHAMA cha ACT Wazalendo mkoa wa Katavi kimelaani kitendo cha uchomaji wa makazi ya watu wanaodhaniwa kuwa wanaishi katika hifadhi ya misitu na kuitaka serikali kutafakari upya  suala hilo.

Katibu wa chama hicho mkoani Katavi Bw.Joseph Mona amesema kuwa visa vya uchomaji wa makazi ya wananchi katika vitongoji kadhaa na kuwaacha bila mahali pakuishi ni suala lisilo kubalika.
Sanjari na hayo ameeleza kuwa mkakati wa chama hicho wa kuishauri serikali ikiwemo kuikosoa umepelekea kuwasilisha ajenda kadhaa za wananchi katika ofisi za mkuu wa mkoa wa Katavi Meja Jeneral  mstaafu Raphael Muhuga kwa ufumbuzi wa tatizo hilo.
Mwanzoni mwa mwezi huu Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Lilian Matinga ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Mpanda amekili kufanyika kwa zoezi hilo kwa madai kuwa limefanywa katika maeneo ambayo wananchi wamevamia misitu.
Vitongoji  vilivyo kumbwa na kadhia ya kuchomewa makazi ni Kitongoji cha Nsanda kilichopo kata ya Kanoge, Makutanio na Mgolokani katika  kata ya Stalike  ambapo mamia ya wakazi wanaishi chini ya miti na familia zao.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA