UGOMVI WA MKULIMA NA MFUGAJI WASABABISHA MAJERUHI KATAVI-Agosti 21,2017

WATU wawili wilayani Mpanda Mkoani Katavi wamejeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao baada ya kuzuka ugomvi uliosababishwa na  kile kilichodaiwa ni kupishana kauli kati ya mkulima na mfugaji katika kijiji cha mbugani kata ya Kakese iliyopo manispaa ya Mpanda.

Katika tukio hilo ambalo limesemekana kusababishwa na ugomvi kati ya mkulima na mfugaji,akijieleza kwa lugha ya kisukuma Bw.Bendi Bubwakala(45) aliyejeruhiwa vibaya katika taya lake la mkono wa kulia alisema yeye hakuwa na ugomvi bali alikuwa akimwambia mfugaji huyo kuwa asogeze ng’ombe mbali na shamba.
Aidha Bw.Bubwakala analalamika pia kushambuliwa na mbwa wa Bw.Daniel John.
Daniel John mtuhumiwa anayedaiwa kumpiga mzee Bubwakala amekana kulisha katika shamba ambapo hata hivyo amekiri kumpiga kwa fimbo na kumjeruhi mzee Bendi Bubwakala wakati wa ugomvi huo alipokuwa akijaribu kujiokoa ambapo kwa upande wake  Daniel John alisema ameshambuliwa na vijana wa mzee Bubwakala baada ya kupigiwa simu.
Kwa upande wake shuhuda wa tukio hilo Bw.Nicholaus Michael amesema ng’ombe walikuwa mbali na shamba tofauti na madai ya Bw. Bendi Bubwakala ambapo pia mbwa jike wa mfugaji Daniel John inasemekana amemshambulia mzee.
Kwa upande wake kaimu Afisa Mtendaji wa kata ya Kakese Bw.Abel Joseph amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi wa kata ya Kakese kutojichukulia sheria mkononi ambapo chanzo cha tukio amesema ni ugomvi kati ya mkulima na mfugaji wakilaumiana kulishiana miwa shambani.
Migogoro ya wakulima na wafugaji katika mkoa wa Katavi imekuwa ikiripotiwa licha ya kuwa siyo kwa kiwango kikubwa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA