WAKAZI TABORA WATAKIWA KUACHA KUTUMIA DAWA KWA MAZOEA



Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora wameshauriwa kujenga utamaduni wa kuhudhuria katika vituo vya kutolea huduma za afya na kuacha kutumia dawa kwa mazoea.
Hayo yameelezwa na Mganga Mkuu wa zahanati ya Moravian Milumbani,Dkt Lameck Kisulila amesema matumizi ya dawa bila utaratibu maalumu ni chanzo cha magonjwa nyemelezi mwilini na hata kusababisha vifo.
Dkt.Kisulila ameitaka jamii kuwa na desturi ya kupima afya wanapougua kwa sababu itasaidia kubaini aina ya ugonjwa na tiba inayohitajika hatua itakayowasaidia kupunguza madhara mengine mwilini yanayotokana na usugu wa dawa.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa mjini Tabora wamesema wanalazimika kutumia dawa bila kupima afya zao wanapougua kutokana na hali ngumu kiuchumi.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA