MANCHESTER CITY YAMUONGEZEA MKATABA DE BRUYNE NA KUMPA MSHAHARA KAMA WA SANCHEZ



Manchester City imeamua kumuongeza kiungo wake wa pembeni Kevin De Bruyne mkataba wa miaka mitano na nusu.

De Bruyne atakuwa akipokea mshahara wa jumla ya pauni 350,000 kwa wiki sawa na ule anaolipwa Alexis Sanchez aliyejiunga na Manchester United akitokea Arsenal.
Lakini mgawanyo wa De Bruyne ni pauni 280,000 ya mshahara kwa wiki pamoja na bonas ya 70,000.
Kiungo huyo wa pembeni mwenye kazi alikuwa akiwaniwa kwa karibu na klabu maarufu duniani ya Real Madrid na inaonekana City wamefanya hivyo kuhakikisha anabaki.
Kwa mkataba huo,sasa De Bruyne atabaki Manchester City hadi mwaka 2023.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA