WAANDISHI WATAKIWA KUANDIKA BILA HOFU



SERIKALI mkoani Rukwa imewataka waandishi wa habari mkoani humo kuyaandika na kuyatangaza mambo mazuri na changamoto zilizopo bila kuhofia mtu yeyote kwani maendeleo ya mkoa huo yatapatikana kwa kuyatangaza mambo yaliyomo katika mkoa huo bila hofu.

Mkuu wa mkoa huo Joachim Wangabo aliwaambia waandishi wa habari wa mkoa huo jana wakati akizindua zoezi la upandaji miti milioni sita lililofanyika juzi katika mji wa Matai wilayani Kalambo.
Alisema kuwa waandishi wa habari ni wadau wakubwa wa maendeleo ya mkoa huo hiyo wanawajibu wa kuandika mambo mazuri na mabaya yaliyopo katika mkoa wa Rukwa kwani kushindwa na kufanikiwa kwa mkoa huo nao kunawahusu.
Wangabo alisema kuwa waandishi wa habari wanatumia kalamu katika kuchangia maendeleo hivyo wajue wanajukumu la kuandika mazuri na changamoto ili mkoa upige hatua kwani wakikaa kimya mkoa ukikosa maendeleo nao itawagharimu.
Alisema kuwa yeye binafsi yupo tayari kuona mkoa wake ukitangazwa kwa mazuri pamoja na changamoto zake kwani ndiyo fursa ya kupiga hatua,na kazi hiyo waandishi wanapaswa kuifanya kwa kuzingatia misingi ya taaluma yao.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka waandishi wa habari kutembea vijijini kuandika habari za uharibifu wa mazingira pamoja na kuhamasisha wananchi wajitume katika kilimo cha kisasa na ufugaji wenye tija kwani mkoa huo unahitaji maendeleo.
Awali akimkaribisha mkuu huyo wa mkoa, mkuu wa wilaya ya Kalambo Juliath Binyura alisema kuwa wananchi wa wilaya ya Kalambo wamejipanga katika kutekeleza zoezi la upandaji miti kwani wanatambua kuwa miti ni uhai.
Alisema kuwa halmashauri ya wilaya hiyo ipo tayari kuwadhibiti watu watakao baininika kuharibu mazingira kwakuwa serikali inatumia fedha nyingi na muda hivyo ni lazima waone thamani ya miti.
Binyura alisema kuwa kwakuwa mkuu wa mkoa amekwisha zindua kampeni ya upandaji miti wananchi wameipokea na wanahakikisha watafikia lengo kwa asilimia mia moja kwani wao ni wakulima na wanahitaji mvua ambayo haiwezi kupatikana bila kuwepo misitu.
Chanzo:Rukwa Kwanza Blog
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA