HALMASHAURI YAAGIZWA KUJENGA MWALO



MKUU wa mkoa wa Rukwa Joachim Wangabo ameiagiza halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga mkoani humo kutafuta fedha ili ijenge mwalo wa Nankanga katika ziwa Rukwa utakao wasaidia wavuvi kufanya biashara ya samaki na utakuwa ni chanzo kizuri cha mapato kwa halmashauri hiyo.

Agizo hilo alilitoa mwishoni wa wiki jana wakati alipokuwa akifanya ziara ya kukagua makambi ya wavuvi wa samaki katika jitihada za kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu uliotokea wilayani humo tangu mwezi Novemba mwaka jana ambapo usababisha vifo vya watu nane na 270 kuugua ugonjwa huo.
Alisema kuwa ufukwe uliopo katika makambi ya wavuvi ya Nankanga katika ziwa Rukwa  wilayani Sumbawanga linafaa kwaajili ya kujenga mwalo ambapo wavuvi watakuwa wanafanya biashara ya samaki na kisha halmashauri kupata fedha kwa kutoza ushuru.
Alisema kuwa wilaya hiyo imejaliwa fursa nyingi ambazo kama zikitumika ipasavyo zitaongeza makusanyo na halmashauri itapata fedha nyingi na itaweza kuwahudumia wananchi ili waaweze kuondokana na changamoto mbalimbali zinazo wakabili.
Alisema kuwa nilazima  itafutwe namna fedha zipatikane haraka na mwalo huo ujengwe kwakuwa wananchi wanahitaji huduma nzuri kwani ni jukumu la watendaji kuzitambua fursa zilizopo na kuzitumia ipasavyo.
Awali akitoa taarifa ya ugonjwa wa kipindupindu katika halmashauri hiyo Kaimu mkurugenzi ambaye ni Mganga mkuu wa wilaya hiyo Fani Musa alisema kuwa kipindupindu kimedhibitiwa licha ya kuwa bado jitihada zinahitajika kutoa elimu ya afya kwa wavuvi.
Alisema kuwa changamoto iliyopo ni kutotumia maji safi na salama kwani baadhi ya wavuvi wanakataa kutumia maji yanayotibiwa kwa dawa aina ya waterguard kwamadai kuwa hayana radha.
Chanzo:Rukwa Kwanza Blog
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA