VIBAKA WATISHIA USALAMA KWA WAKAZI WILAYANI MPANDA MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald
Baadhi ya Wananchi kata ya Misukumilo Manispaa ya Mpanda wamedai kuingiwa na hofu kufuatia kukithiri kwa matukio ya kiharifu katika eneo la linalofahamika kwa jina la Migazini.
Wakazi hao wamesema vitendo vya kiharifu katika eneo la migazini vimekithiri na hivyo kuliomba jeshi la polisi kushughulikia tatizo hilo.
Wametaja uporaji wa mali za nyumbani na kukabwa njiani kasha kunyang’anywa mali ni miongoni mwa matukio yanayofanywa na vibaka hao.
Afisa mtendaji wa kata hiyo Pasca Mbete amekili kuwepo kwa vitendo hivyo na kuahidi kuimarisha ulinzi na usalama ili kuondoa adha hiyo.
Kwa upande wa Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Katavi Damasi Nyanda amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kuwabaini waharifu hao.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA