KIJIJI CHA MTAMBO WILAYANI MPANDA CHATOKOMEZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO

Na.Issack Gerald
Kijiji cha Mtambo kilichopo kata ya Katumba Wilayani Mpanda Mkoani Katavi,kimefanikiwa kutokomeza vifo vya akina mama na watoto.
Hatua hiyo imethibitishwa na Katibu wa Kijiji cha Mtambo Bw.Fenias Fulujensi wakati akijibu malalamiko ya baadhi ya wananchi wanaolalamika kutozwa faini ya shilingi elfu ishirini kutoka kwa wananchi ambao wake zao wanaojifungulia nyumbani.
Bw.Fulujensi amesema katika kipindi cha mwaka 2016 mpaka 2017 wanawake watatu wamefariki dunia kutokana na kuchelewa kufika katika vituo vya huduma za afya ambapo kwa sasa hakuna ripoti ya vifo hivyo.
Hata hivyo Kamimu afisa mtendaji wa Kata ya Katumba Bi.Lucy Kagine ameunga mkono faini hiyo japo amesema hana taarifa ya uwepo wa faini hiyo katika kijiji hicho.
Kwa mjibu wa mwenyekiti wa Kamati ya zahanati ya kijiji cha Mtambo Bw.Karoli Shaltiel amesema kwa kushirikiana na Halmashauri ya serikali ya kijiji cha Mtambo imechukua hatua ya kutunga sheria ndogondogo za kutoza faini baada ya kuonekana asilimia 60 ya akina mama wanajifungulia nyumani hali ambayo imesababisha vifo kwa mama na mtoto.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA