JESHI LA POLISI MKOANI PWANI BADO HALINA TAARIFA ZA KUWEZESHA KUPATIKANA MWANDISHI WA HABARI ALIYEPOTEA KATIKA MAZINGIRA YA KUTATANISHA

Na.Issack Gerald
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani limesema mpaka sasa halina taarifa za kutosha zinazowezesha kupatikana mwandishi wa gazeti la mwananchi Azori Gwanda aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha siku 18 zilizopita.
Kauli hiyo imetolewa na kamanda wa Jeshi hilo Mkoani Pwani Kashmishna Msaidizi Jonathani Shana ambapo amewataka wananchi wenye taarifa muhimu kuhusu tukio hilo walitaarifu jeshi la polisi ili lizifanyie kazi.
Katika hatua nyingine,Kamanda Shana amesema siyo miili yote ilioonekana ikielezea katika habari ya hindi miezi michache iliyopita inahusishwa na utekaji bali pia imebainika hata matukio ya ajali,upepo na uzembe wa baadhi ya wahanga vinahusika.
Mkoa wa Pwani ni Mkoa ambao umekubwa na matukio watu kupigwa risasi na kuuwawa na watu wasiojulikana wakiwemo viongozi wa serikali za mitaa na maafisa wa polisi hali ambayo imesababishwa kuanzishwa mkoa wa kipolisi Mkoani Pwani kama njia mojawapo ya kudhibiti matukio hayo.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA