WATOTO WALIOKUWA WAMEPOTELEA MSITUNI MKOANI KATAVI WAMEPATIKANA WAKIWA HAI.

Na.Issack Gerald
Baadhi ya wakazi wa Kata ya Katumba Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,wamekipongeza kituo cha Mpanda Radio kwa kusaidia juhudi za kupatikana kwa watoto wawili waliokuwa wamepotea katika mazingira ya kutatanisha.
Wakazi hao wakiwemo Bw.Alex Gezaho,wamesema siku chache baada ya Mpanda Radio Kutangaza upotevu wa watoto hao wanaojulikana kwa majina ya Rama na Vitisho walipatikana porini wakiwa na afya njema.
Kwa mjibu wa taarifa zilizokuwa zimetolewa na viongozi wa Kijiji cha Mnyaki,watoto hao walikuwa wamepotea wakati wakiwinda ndege porini kwa manati karibu wiki mbili zilizopita.
Kumekuwa na matukio ya upotevu wa watoto kata ya Katumba ambapo kwa mjibu wa viongozi wa serikali ya Kijiji cha Mnyaki pamoja na wananchi,mtoto mmoja aliyepotea miaka mitano iliyopita hakupatikana mpaka sasa hatua ambayo kupatikana kwa watoto Rama na Vitisho limepokelewa kwa furaha.

Source: Issack Gerald,Editor:Issack Gerald

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA