KAULI YA SERIKALI MANISPAA YA MPANDA IMEWASIKITISHA WATU WENYE ULEMAVU MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald
Watu wenye ulemavu Mkoani Katavi,wameeleza kusikitishwa na kauli ya serikali kuwa haina pesa za kuwawezesha kufanya maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani.
Masikitiko hayo wameyatoa leo katika kikao cha kupanga tarehe nyingine ya maadhimisho ambapo wamepanga yafanyike Desemba 19 mwaka huu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu SHIVYAWATA Mkoani Katavi Issack Mlela amesema serikali kutowawezesha kufanya maadhimisho ni kutowatendea haki wakati serikali inasema mapato yameongezeka serikalini.
Juzi Afisa maendeleo ya jamii Bi.Marietha Mlozi na Afisa Ustawi wa jamii Bi.Agness Bulaganya wote wa Manispaa ya Mpanda walikuwa wameiambia Mpanda Radio kuwa maadhimisho ya siku ya Watu wenye ulemavu yangefanyika Desemba 3 ambayo hata hivyo yameahirishwa baada ya ukosefu wa pesa.
Haki za watu wenye ulemavu zinasimamiwa na sheria mbalimbli ikiwemo sheria namba 9 ya mwaka 2010 inayitaka serikali na jamii kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapatiwa haki katika masuala yote muhimu hasa katika elimu,afya,kuishi na haki nyingine za kibinadamu ambapo pia Tanzania ni miongoni mwa taifa katika jumuiya ya madola iliyosaini mikataba mbalimbali ili kuhakikisha haki za watu wenye ulemavu zinapatikana kama wasio na ulemavu wanavyohudumiwa ambapo kama nchi haitekelezi haki hizi ni kumnyima haki mtu mwenye ulemavu.
Maadhimisho ya mwaka huu kitaifa yamefanyika Mkoani Simiyu na kaulimbiyu ikisema ‘’Badilika kuelekea jamii jumuishi na imara kwa wote’’.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA