WIZARA YATOA TAMKO KWA WALIOPOTEZA VYETI VYAO VYA ELIMU

Wizara ya Elimu,Sayansi,Teknolojia imewataka watanzania wote nchini waliopoteza vyeti vyao vya elimu watoe taarifa mapema katika sehemu husika na wasisubiri mpaka pale wanapokuwa na uhitaji navyo ndio waanze kuhangaika.

Mhe.William Ole Nasha
Hayo yameelezwa leo Bungeni na Naibu Waziri Wizara ya hiyo Mhe.William Ole Nasha kwa niaba ya Waziri ya Waziri Sayansi,Teknolojia wakati alipokuwa anajibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato David Chumi.
Chumi alitaka kufahamu serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Elimu ina mpango gani wa kuwasaidia watanzania waliopoteza vyeti vyao vya elimu na kuvipata vingine.
Kwa upande mwingine,Mhe.William Ole Nasha amesema muombaji wa cheti mbadala au uthibitisho wa matokeo hupatiwa huduma baada ya kumaliza utaratibu wote uliyowekwa na Wizara hiyo.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA