CWT KATAVI CHAMPONGEZA RAIS MAGUFULI KUTENGA SHILINGI BIL.200 KULIPA MADENI YA WATUMISHI

Chama cha Walimu CWT mkoa wa Katavi kimempongeza rais wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa kutangaza kutoa fedha Shilingi bilioni 200 ili zilipe madeni ya ndani yakiwemo ya walimu.
Kauli ya pongezi imetolewa na katibu wa chama hicho mwalimu Hamis Chinahova ambapo amesema hatua ya serikali kulipa madeni hayo italeta mageuzi makubwa katika sekta ya elimu.
Katika hatua nyingine amewataka waalimu kuendelea kujituma na kufanya kazi kwa weledi zaidi ili kuleta tija kwa jamii na taifa kwa ujumla.
Mwaka 2017 walimu nchini Tanzania walitishia kugoma kwa kile walichokitaja kuwa ni kukithiri kwa madai dhidi ya serikali wakisema inawavunja molali ya kufanya kazi.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA