MBUNGE KAPUFI WA MPANDA AUNGURUMA BUNGENI TOZO ZA ZIMAMOTO

Na.Issack Gerald
Serikali  imesema tozo inayotozwa na jeshi la zima moto na uokoaji kwa lengo la kutoa kibali cha ujenzi ni kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2015.
Katika picha Mh.Sebastian Kapufi anayesalimiana na waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Ufafanuzi huo umetolewa leo na Naibu waziri wa Wizara ya mambo ya ndani ya nchi  ambapo amesema awali sheria hiyo ilikuwa haifuatwi ila kwa sasa utekelezaji umeanza na hivyo kila mwananchi anatakiwa kutii sheria hiyo.
Kauli ya Waziri Naibu Waziri-Mhandisi Hamad Yusuf Masauni wakati Akijibu swali la mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Sebastiani Simoni Kapufi aliyetaka kujua  kama tozo hizo zipo kihalali.
Aidha naibu waziri amesema ili kuondokana na majanga yanayotokana na ujenzi holela lazima wananchi walipie tozo hiyo ili wapate kibali cha ujenzi.
Wiki iliyopita,Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Katavi wiki lilitangaza kushuka kwa bei ya tozo hiyo kutoka shilingi 150,000/=na kufikia 50,000/= ili kila wananchi amudu gharama.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA