ASKARI WA WANYAMA PORI MKOANI ARUSHA WAMEINGIA MGOGORO NA WAFUGAJI


Na Geofrey Stephen-Arusha.

Wakazi wa kata za Ololosokwan,Soitsambu wilayani Ngorongoro mkoani Arusha,wamewashutumu baadhi ya askari wa mamlaka ya hifadhi ya Serengeti(Senapa) kukamata mifugo yao katika ardhi za vijiji na kisha kuipeleka ndani ya hifadhi.
Moja ya alama inayotambulisha Mkoa wa Arusha
Mwenyekiti wa kijiji cha Kirtalo,Yohana Toroge amesema,jumla ya ng’ombe wake 1000 walikamatwa   Novemba 4 mwaka huu  wakati wakielekea kunywa maji kisimamani na kisha kupelekwa ndani ya maeneo ya hifadhi.

Aidha Wakazi hao walitoa kilio chao mbele ya waandishi wa habari katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Olosokwan uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kimila.
Mkuu wa mamlaka ya hifadhi ya Serengeti (Senapa), William Mwakilema alijibu shutuma hizo na kusema wakazi hao wanatunga uongo kwa kuwa hakuna askari wake  anayekamata mifugo ndani ya ardhi za vijiji na kuwalipisha faini kubwa.
Wenyekiti wa halmashauri ya Ngorongoro,Mathew Siloma amesema wao kama halmashauri wanapinga vikali vitendo vya baadhi ya askari wa Senapa kukamata mifugo ndani ya makazi ya watu.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA