KIJANA AMEUAWA AKIIBA MIHOGO MKOANI RUKWA

KIJANA aliyetambulika kwa jina la zakaria Katembo (30) mkazi wa kijiji cha Kakoma Kata ya Kipundu  wilayani Nkasi mkoani Rukwa,ameuawa kwa kupigwa mpini na watu wasiojulika na wanaodaiwa kuwa na hasira kali.
Mwenyekiti wa kijiji cha Kakoma  Patrick Mwami alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 4 za usiku baada ya wananchi wa kijiji hicho wanaodaiwa kuwa na hasira Kali kumvamia kijana huyo akiwa shambani alikokuwa akichimba mihogo na kumuua kwa kipigo.
Alisema wananchi baada ya kufanya mauaji hayo waliuacha mwili wa marehemu huyo katika shamba hilo na kuondoka na hawakubainika ni wakina nani waliofanya tukio hilo.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Kipundu John Kapandila amesema  baada ya tukio hilo aliutaka uongozi wa kijiji kutoa taarifa polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Aidha aliitaka jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi badala yake wafuate sheria ili iweze kuchukua mkondo wake katika kuwaadhibu wahalifu.
Kwau pande wake mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilayani Nkasi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Said mtanda alisema watawasaka wote waliofanya mauaji hayo na kuwabaini ili sheria ichukue mkondo wake. 
Naye Kamanda wa Polisi mkoani humo George Kyando alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema polisi wanaendelea na uchunguzi ili kuwabaini watuhumiwa wa mauaji hayo ili wafikishwe kizimbani wakajibu tuhuma zitakazo wakabili. 
Hata hivyo alionya tabia ya baadhi ya wananchi kujichukulia sheria mikononi kwani kufanya hivyo ni makosa na lazima wanaofanya hivyo wachukuliwe hatua kali ili kukomesha mauaji holela. 
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA