CWT MKOANI RUKWA:WALIMU TIMIZENI WAJIBU WENU KABLA YA KUDAI HAKI

KIMCHAMA cha walimu CWT wilayani Kalambo mkoani Rukwa kimewataka walimu kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kabla ya kudai haki mbalimbali ikiwemo nyongeza ya mshahara.
Ushauri huo umetolewa na katibu wa chama hicho Peter Simwanza wakati wa sherehe maalumu za kuwapongeza walimu wa shule za msingi zilizopo katika kata ya Ulumi ambao wanafunzi wao walifaulu vizuri kwa kupata kiwango cha alama A katika masomo ya kuhitimu darasa la saba pamoja na shule zilizofanya vizuri.
Alisema baadhi ya walimu wamekuwa mbele katika kudai haki zao mbalimbali ikiwemo nyongeza ya mshahara lakini hawatimizi wajibu wao kwamujibu wa sheria. 
Simwanza alisema walimu wilayani humo wanapaswa kutekeleza sheria zote za kazi kwa mujibu wa mkataba wa ajira ndipo wadai haki zao kwa mwajiri. 
Katika hatua nyingine,aliwataka walimu kutokuwa wanyonge wanapoona haki zao zimekiukwa kwa kuwa maslahi yao yapo mikononi mwao lakini kwa kufuata sheria,kanuni na taratibu. 
Naye Sabina Mwamwezi mwakilishi wa walimu kitengo cha wanawake katika chama hicho aliwasihi walimu wa kike wilayani humo kuhakikisha wanajali haiba katika suala la mavazi ili kulinda maadili ya wanafunzi. 
Kwa upande wake mwalimu Zainab Omary wa shule ya msingi Ulumi ambaye wanafunzi walipata alama A wengi katika somo analofundisha la kiswahili alisema mafanikio makubwa yalitokana na yeye binafsi kulipenda somo hilo sambamba na kujituma katika kufundisha pia kuwapenda wanafunzi wake. 
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA