WAFANYABIASHARA KATAVI WAREJESHEWA FEDHA ZAO WALIZOTAPELIWA


Katibu wa jumuiya ya wafanyabiashara Tanzania mkoani Katavi Bw.Robison Thompson Bumela amethibitisha fedha za kurejeshwa kwa wafanyabiashara waliokuwa wakidai kutapeliwa na baadhi ya makambuni yanayouza mashine za kielektronic (EFDs) hapa nchini.

Hatu hiyo meithibitisha leo Ofisini kwake wakati akizungumza na mwandishi wetu kuhusu hatima ya malalamiko ya wafanyabiasahara waliokuwa wakidai kutapeliwa fedha bila kupata mashine hizo.
Aidha Bw.Bumela amesema wafanyabiashara wachache ambao hawajarejeshejewa pesa zao ni waliokuwa wamelipia bila kupewa risiti na hivyo kuleta ugumu katika ushahidi ili kumbana wakala aliyechuku fedha zao.
Hata hivyo katibu huyo amebainisha kuwa miongoni mwa changamoto zilizopo katika matumizi ya mashine ya EFDs ni mashine hizo kutotunza kumbukumbu kwa muda mrefu hali inayosababisha kumbukumbu kupotea baada ya kufutika.
Kupitia mikutano mbalimbali ya wafanyabiashara,Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Bi.Lilian Matinga walikuwa akiiagiza mamlaka ya ya Mpato Tanzania TRA Mkoani Katavi kuhakikisha wafanyabiashara wanapata fedha au mashine zao za EFDs kwa kuwa mawakala walikuwa wakifanya kazi hiyo kwa kushirikiana na ofisi za TRA Mkoa.
Jumuiya hiyo iliyoanzishwa mwaka 2014 kwa sasa ina wafanyabisahara wanachama zaidi ya 150 ambapo zaidi ya wafanyabiasahara 10 walikuwa wametapeliwa na makampuni yanayojinasibu kuwa yanauza mashine za EFDs miaka miwili iliyopita.
Kwa mjibu wa wafanyabiashara.mashine moja bei yake ni mpaka shilingi laki 8.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA