RAIS MAGUFULI ATEUA MABALOZI WAWILI YUMO IGP MSTAAFU KUAPISHWA HIVI PUNDE



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli leo atawaapisha Mabalozi Wateule wawili aliowateua kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Rwanda na Urusi.
Rais Magufuli akiwa na IGP Mstaafu Ernes Jumbe Mangu
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mhe.Rais Magufuli atamuapisha IGP-Mstaafu Ernest Jumbe Mangu kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda.
Aidha amesema Meja Jenerali Mstaafu Simon Marco Mumwi ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Urusi.
Hafla ya kuapishwa kwa Mabalozi Wateule hao inatarajia kufanyika hivi punde kuanzia majiara ya saa 5:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Uteuzi huo ulifanyika jana Machi 20,2018

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA