UVAMIZI NA UNYANG’ANYI WA PIKIPIKI MKOANI KATAVI

Na.Issack Gerald
Mtu mmoja anayefahamika kwa jina Korode Merikiolo mkazi wa kata ya Katumba Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,amevamiwa usiku wa kuamkia leo na kunyang’anywa pikpiki aliyokuwa akiendesha akitokea soko la Mnyaki huku akishambuliwa na watu wawili ambao hawajatambulika.
Bw.Korode Merikiolo pamoja na kusema kuwa alipgwa sehemu mbalimbali za mwili wake,amesema wakati wanatekwa na kunyang’anywa pikipiki alikuwa amembeba Lea Bitabo ambapo msichana huyo amesema wakati akitaka kukimbia alizuiliwa na wanyang’anyi hao.
Mwenyekiti wa kijiji cha Mnyaki B Bw.Yusto Zambayembi kwa upande wake amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema alipokea taarifa hizo saa 3 usiku.
Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi amethibitisha kupokea taarifa za tukio hilo.
Hata hivyo licha ya  matukio ya watu kuvamiwa, kujeruhiwa na kunyang’anywa mali zao kutokea na kuripotiwa katika kituo cha polisi Katumba na wengine kutibiwa katika kituo cha afya Katumba,Kamanda wa POlisi Damasi Nyanda amekana kuwa na taarifa za matukio hayo.
Takribani wiki mbili zilizopita,matukuio ya watu kuvamiwa nyakati za usiku na kuporwa mali zao yalitokea ambapo moja na tukio ni mmoja wa wakazi kuvamiwa na kuibiwa fedha na mali zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja ambapo katika kipindi hicho matukio yapatayo matatu yameripotiwa.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA